|
|
|
|
|
Enzi ya Shang |
|
中国国际广播电台
Wataalamu husika wanaona kuwa
Xia ni enzi ya kifalme ya zamani
zaidi nchini China, lakini takwimu
husika za kihistoria kuhusu
enzi ya Xia, lakini hadi hivi
sasa bado hazijathibitishwa
na mabaki ya kale isipokuwa
kuelezwa na maandishi ya vizazi
vilivyofuatia. Enzi ya kwanza
katika zamani za kale nchini
China, ambayo imethibitishwa
na mabaki ya kale ni enzi ya
kifalme ya Shang. Enzi ya Sahgn
iliyodumu kwa kiasi cha miaka
600, iliasisiwa katika karne
ya 16 kabla ya Kristu na iliangamia
katika karne 11 kabla ya Kristu.
Enzi ya Shang ilihamisha mji
mkuu mara kadhaa, na mara ya
mwisho mji mkuu ulihamishwa
hadi mji wa Yin, ambao ni karibu
na mji wa Anyang, mkoa wa Henan
wa hivi sasa. Mabaki ya kale
yaliyofukuliwa kutoka ardhini
yamethibitisha kuwa katika kipindi
cha mwanzo cha enzi ya Shang,
ustaarabu wa China ulikuwa umeendelezwa
kwenye kiwango cha juu, ikiwa
ni pamoja na utamaduni wa maandishi
yaliyochongwa kwenye magamba
ya kobe na vyombo vya shaba
nyeusi. Magofu ya mji wa Yin,
ambayo yaligunduliwa mwaka 1928,
ni ugunduzi mkubwa kuhusu mabaki
ya kale nchini China katika
karne 20. Baada ya hapo mabaki
mengi yenye thamani yalifukuliwa
kwa wingi.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|