Enzi ya Shang
中国国际广播电台
Wataalamu husika wanaona kuwa Xia ni enzi ya kifalme ya zamani zaidi nchini China, lakini takwimu husika za kihistoria kuhusu enzi ya Xia, lakini hadi hivi sasa bado hazijathibitishwa na mabaki ya kale isipokuwa kuelezwa na maandishi ya vizazi vilivyofuatia. Enzi ya kwanza katika zamani za kale nchini China, ambayo imethibitishwa na mabaki ya kale ni enzi ya kifalme ya Shang. Enzi ya Sahgn iliyodumu kwa kiasi cha miaka 600, iliasisiwa katika karne ya 16 kabla ya Kristu na iliangamia katika karne 11 kabla ya Kristu. Enzi ya Shang ilihamisha mji mkuu mara kadhaa, na mara ya mwisho mji mkuu ulihamishwa hadi mji wa Yin, ambao ni karibu na mji wa Anyang, mkoa wa Henan wa hivi sasa. Mabaki ya kale yaliyofukuliwa kutoka ardhini yamethibitisha kuwa katika kipindi cha mwanzo cha enzi ya Shang, ustaarabu wa China ulikuwa umeendelezwa kwenye kiwango cha juu, ikiwa ni pamoja na utamaduni wa maandishi yaliyochongwa kwenye magamba ya kobe na vyombo vya shaba nyeusi. Magofu ya mji wa Yin, ambayo yaligunduliwa mwaka 1928, ni ugunduzi mkubwa kuhusu mabaki ya kale nchini China katika karne 20. Baada ya hapo mabaki mengi yenye thamani yalifukuliwa kwa wingi.