Enzi ya Zhou ya Magharibi
中国国际广播电台
Zhou ni enzi ya tatu baada ya enzi ya Xia na Shang nchini China katika zamani za kale. Enzi ya Zhou, ambayo ilidumu kwa miaka zaidi ya 770, ilianzishwa mwaka 1027 kabla ya Kristu na kuangushwa na nchi ya Qing mwaka 256 kabla ya Kristu. Kabla ya mji mkuu kuhamia kwa upande wa mashariki, nchi hiyo iliitwa kuwa Zhou ya magharibi, na kuitwa Zhou ya mashariki baada ya mji mkuu wa nchi kuhamia kwa upande wa mashariki. Enzi ya Zhou ya mashariki iligawanyika katika vipindi viwili vya Chunqiou na Zhanguo.

Baada ya mji mkuu kuhamia mji wa Gao ulioko sehemu ya mashariki, mfalme wa kwanza wa enzi ya Zhou aliyejulikana kwa Wu aliongoza majeshi kushambulia enzi ya Shang na kuasisi enzi ya kifalme ya Zhou.

Mwaka 770 wa kabla ya Kristu hadi mwaka 476 wa kabla ya Kristu ilikuwa enzi ya Chunqiu. Pamoja na ongezeko la idadi ya watu na maendeleo ya uchumi, yalizushwa mapigano makali ya kugombea umiliki kati ya nchi kubwa. Hali ya jamii ilitokewa na mabadiliko makubwa. Katika uzalishaji wa kilimo, wakulima walianza kutumia vyombo vya kilimo vilivyotengenezwa kwa chuma, kutumia ng’ombe kulima mashamba na kujenga miradi ya maji, hatua hiyo iliongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo. Chunqiu ni kipindi cha mpito ambapo utaratibu wa jadi wa kisiasa na kijamii wa Zhou ya magharibi ulisambaratika hatua kwa hatua.

Confucius, ambaye alikuwa mwana nadharia mkubwa na mwanaelimu mkubwa nchini China, alizaliwa katika kipindi cha mwisho cha Chunqiu. Kwenye msingi wa kujumlisha utamaduni na mawazo ya zamani, Confucius akifikiria hali halisi ya jamii yenye mgogoro, alitoa mfumo wa maoni ya nadharia kuhusu utu, uadilifu na masuala ya kijamii na kisiasa, na kuanzisha kundi la wasomi wenye mawazo ya confucius katika zamani za kale.

Kipindi cha Zhanguo (toka mwaka 403 kabla ya Kristu hadi mwaka 221 kabla ya Kristu) ni kipindi ambacho watawala wa sehemu mbalimbali nchini waligombea madaraka baada ya Zhou ya mashariki. Katika kipindi hiki, mabadiliko makubwa yalitokea nchini China: nchi nyingi ndogo ndogo zilimezwa na nchi kubwa na hatimaye zikabaki nchi 7 kubwa. Katika kipindi hicho, nchi mbalimbali zilifanya mageuzi, hususan nchi ya Qin.

Ingawa katika kipindi cha Zhanguo zilitokea vita mwaka hadi mwaka, lakini hali hiyo haikuathiri maendeleo ya utamaduni wa kale nchini China, shughuli za kundi la watu wenye elimu kubwa walistawisha utamaduni wa fani maalumu. Katika kipindi hicho utamaduni wa mawazo ulifikia kileleni katika historia ya kale ya China yakiwemo makundi ya Confucius na Menfucius; kundi la kidao lililowakilishwa na Laozi, Zhuangzi na Liezi; kundi la wanasheria lililowakilishwa na Hanfei; na kundi la Mozi, makundi hayo yaliungwa mkono na kuheshimiwa na vizazi vya baadaye. Hali ya kuweko kwa makundi yenye mawazo tofauti yalihimiza maendeleo ya siasa na uchumi kwa wakati ule, tena inaendelea hadi hivi sasa.

Mwaka 230, mfalme Yingzheng wa enzi ya Qin akitumia muda wa miaka 9 aliangusha nchi nyingine 6 na kuunganisha sehemu zote za China katika mwaka 230 kabla ya Kristu. Hadi hapo hali ya mfarakano uliodumu kwa karibu miaka 600 ilimalizika.