|
|
|
|
|
Qin-Enzi ya Kwanza ya Kimwinyi |
|
中国国际广播电台
Baada ya kupita miaka zaidi
ya 2,000 ya jamii yenye utaratibu
wa umilikaji wa watumwa, enzi
ya kwanza ya kimwinyi nchini
China iliasisiwa mwaka 221 kabla
ya Kristu. Kuasisiwa enzi ya
Qin kuna maana muhimu katika
historia ya China. Mwaka 255
hadi mwaka 222 kabla ya Kristu
China iliingia katika kipindi
cha mwisho cha jamii yenye utaratibu
wa umilikaji wa watumwa. Wakati
ule kulikuwa na nchi nyingi
ndogo ndogo, ambazo zilipigana
vita, hatimaye zikabaki nchi
7 kubwa. Enzi ya Qin kati ya
nchi hizo 7, iko katika sehemu
ya kaskazini magharibi, ilifanya
mapema mageuzi ya kijeshi na
kilimo, ambapo nguvu ya Qin
iliimarika. Mwaka 247 kabla
ya Kristu, Ying Zheng mwenye
umri wa miaka 13 alirithi ufalme,
alipoanza kutawala alipotimiza
umri wa miaka 22, alianza kutekeleza
mpango wake wa kuteka nchi nyingine
6. katika muda wa miaka 10 kutoka
mwaka 230 kabla ya Kristu hadi
mwaka 221 kabla ya kristu mfalme
Yingzheng aliangusha nchi nyingine
6 na kuunganisha sehemu zote
za China. Kuunganishwa kwa sehemu
zote nchini na kuimarisha umoja
wa China kulikuwa na maana muhimu
katika historia ya China. Kwanza
mfalme Yingzheng alianzisha
serikali za mitaa ambazo ni
pamoja na mikoa 36 na wilaya
zake ambazo baadhi ya majina
yake yanatumika hadi hivi sasa.
Pili, mchango mkubwa uliotolewa
na enzi ya Qin ni kutumia maneno
ya aina moja, hatua ambayo ilichangia
urithi wa utamaduni wa China.
Tatu, ulianzishwa utaratibu
wa upimaji wa namna moja kote
nchini ikiwa ni pamoja na upimaji
wa urefu, ujazo, ukubwa na uzito,
hatua hiyo ilianzisha mazingira
bora kwa maendeleo ya uchumi
wa nchi, hali kadhalika kwa
uimarishaji wa hadhi ya utawala
wa serikali kuu. Mfalme Yingzheng
aliunganisha sehemu zote za
China na kumaliza hali ya mfarakano
na kujenga nchi kubwa ya kimwinyi
yenye makabila mengi, ambayo
kabila la wahan ni uti wa mgongo
na kufungua ukurasa mpya wa
historia.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|