Qin-Enzi ya Kwanza ya Kimwinyi
中国国际广播电台
Baada ya kupita miaka zaidi ya 2,000 ya jamii yenye utaratibu wa umilikaji wa watumwa, enzi ya kwanza ya kimwinyi nchini China iliasisiwa mwaka 221 kabla ya Kristu. Kuasisiwa enzi ya Qin kuna maana muhimu katika historia ya China. Mwaka 255 hadi mwaka 222 kabla ya Kristu China iliingia katika kipindi cha mwisho cha jamii yenye utaratibu wa umilikaji wa watumwa. Wakati ule kulikuwa na nchi nyingi ndogo ndogo, ambazo zilipigana vita, hatimaye zikabaki nchi 7 kubwa. Enzi ya Qin kati ya nchi hizo 7, iko katika sehemu ya kaskazini magharibi, ilifanya mapema mageuzi ya kijeshi na kilimo, ambapo nguvu ya Qin iliimarika. Mwaka 247 kabla ya Kristu, Ying Zheng mwenye umri wa miaka 13 alirithi ufalme, alipoanza kutawala alipotimiza umri wa miaka 22, alianza kutekeleza mpango wake wa kuteka nchi nyingine 6. katika muda wa miaka 10 kutoka mwaka 230 kabla ya Kristu hadi mwaka 221 kabla ya kristu mfalme Yingzheng aliangusha nchi nyingine 6 na kuunganisha sehemu zote za China. Kuunganishwa kwa sehemu zote nchini na kuimarisha umoja wa China kulikuwa na maana muhimu katika historia ya China. Kwanza mfalme Yingzheng alianzisha serikali za mitaa ambazo ni pamoja na mikoa 36 na wilaya zake ambazo baadhi ya majina yake yanatumika hadi hivi sasa. Pili, mchango mkubwa uliotolewa na enzi ya Qin ni kutumia maneno ya aina moja, hatua ambayo ilichangia urithi wa utamaduni wa China. Tatu, ulianzishwa utaratibu wa upimaji wa namna moja kote nchini ikiwa ni pamoja na upimaji wa urefu, ujazo, ukubwa na uzito, hatua hiyo ilianzisha mazingira bora kwa maendeleo ya uchumi wa nchi, hali kadhalika kwa uimarishaji wa hadhi ya utawala wa serikali kuu. Mfalme Yingzheng aliunganisha sehemu zote za China na kumaliza hali ya mfarakano na kujenga nchi kubwa ya kimwinyi yenye makabila mengi, ambayo kabila la wahan ni uti wa mgongo na kufungua ukurasa mpya wa historia.