Kabila la Wahan
中国国际广播电台
Mwaka 206 kabla ya Kristu hadi mwaka wa 8 ni kipindi cha enzi ya Han ya magharibi katika historia ya China. Liu Bang ambaye aliyekuwa mfalme Gao aliasisi enzi ya Han na kuchagua Changan kuwa mji mkuu.

Katika miaka ambayo mfalme Hangaozu alikuwa madarakani, aliimarisha utawala wa serikali kuu na kubuni sera za kuboresha maisha ya wananchi. Mwaka 159 kabla ya Kristu, mfalme Hangaozu alifariki, Hui alirithi ufalme wake, lakini wakati ule madaraka ya serikali, yalikuwa mkononi mwa malkia Lu, ambaye ni mke wa mfalme Hangao. Malkia Lu alitawala kwa miaka 16, na ni mmoja wa watawala wachache wa wanawake katika historia ya China. Mwaka 183 kabla ya Kristu, Wen alirithi ufalme, yeye na mtoto wake ambaye alirithi ufalme (toka mwaka 156 kabla ya Kristu hadi mwaka 159 kabla ya Kristu) waliendelea kutekeleza sera za kuboresha maisha ya wananchi, kupunguza kodi na kukuza uchumi wa nchi.

Kutokana na sera bora za wafalme wa hao, nguvu ya enzi ya Han iliimarika. Mwaka 141 kabla ya Kristu Wu alirithi ufalme na kutuma Wei Qing na Huo Qubing kwenda kupigana vita na kabila la waxiongnu, hatimaye walishinda vita na kupanua ardhi ya enzi ya Han ya magharibi, na kufanya uchumi na utamaduni kupata maendeleo katika sehemu ya kaskazini.

Kutokana na kutekelezwa kwa sera za kukuza uzalishaji mali na kuboresha maisha ya wananchi, nguvu ya enzi ya Han iliimarika, lakini katika wakati huo huo, nguvu ya mikoa pia iliimarika ha kuhatarisha utawala wa kifalme. Mwaka wa 8 baada ya Kristu, Wang Mang alijinyakulia ufalme na kuasisi enzi ya Xin.

Enzi ya Han ya magharibi ni moja ya enzi yenye nguvu kubwa katika historia ya China, hivyo enzi ya Han ilikuwa katika hali ya utulivu kwa miaka yote ya utawala wake. Mfalme Wu alisikiliza pendekezo la waziri Dong Zhognshu la “kuacha nadharia nyingine na kuheshimu nadharia ya Confucius peke yake.” Tokea hapo, nadharia na elimu ya Confucius vikawa sera za kutawala kwa enzi zote zilizofuata.

Tokea mwaka 25 hadi mwaka 220 ni kipindi cha enzi ya Han ya mashariki, ambayo iliasisiwa na Liu Xiu ambaye alijiita mfalme Guangwu.

Katika miaka ya mwanzo ya enzi ya Han ya mashariki, utawala wa serikali kuu uliimarisha maelewano na utawala wa kikanda, utawala wa nchi ulielekea hali ya utulivi, kiwango cha uchumi, utamaduni, sayansi na teknolojia kilizidi kile cha enzi ya Han ya magharibi. Mwaka 105 Cai Lun alivumbua teknolojia ya utengenezaji wa karatasi. Katika upande wa sayansi ya kimaumbile, Zhang Heng alivumbua zana za kuchunguza hali ya sayari na tetemeko la ardhi. Katika kipindi cha mwisho cha enzi ya Han ya mashariki, dakatari Hua Tuo alifanya upasuaji kwa wagonjwa kwa kutumia dawa ya nusukaputi.