Nchi za Wei, Jin na Enzi za Kusini na Kaskazini
中国国际广播电台
Kipindi cha Wei na Jin (mwaka 220 hadi mwaka 589) mwishoni mwa karne ya 2, utawala wa Han ya mashariki ulizorota, historia ya China iliingia kipindi cha muda mrefu cha mfarakano. Mwanzoni ni nchi tatu zilizokabiliana za Wei, Shu na Wu (mwaka 189 hadi mwaka 265), hali hiyo ya kukabiliana ilimalizwa na Jin ya magharibi, lakini umoja wa Jin ya magharibi ulidumu kwa muda mfupi (mwaka 265 hadi mwaka 316), hali ya mfarakano ikatokea tena. Jamaa za mfalme wa Jin ya magharibi walianzisha nchi ya Jin ya mashariki (mwaka 317 hadi mwaka 420), mgogoro wa mapigano ulitokea katika sehemu ya kaskazini, ambapo zilianzishwa nchi 16.

Katika kipindi hicho, uchumi wa sehemu ya kusini ulikuwa na maendeleo makubwa. Makabila yaliyokuwa katika sehemu za magharibi na kaskazini yalihamia sehemu ya kati kwa mfululizo, ambapo uhamiaji na kuishi kwa kuchanganyika pamoja vilihimiza kuungana na kuingiliana. Katika upande wa utamaduni, elimu kuhusu uhai ilienea kwa haraka, ambapo dini za kibudha na kidao zilikuzwa katika mgongano, lakini kwa kawaida watawala walilinda dini ya kibudha. Katika upande wa fasihi na sanaa kulikuwa na maandishi na mashairi mengi, michoro ya sanaa iliyoko katika mapango ya mawe ya Denghuang ni sanaa murua ya kudumu.

Katika upande wa sayansi na teknolojia, Zu Chongzhi alikuwa mtu wa kwanza aliyefanya hesabu kuhusu ulinganifu kati ya mzingo wa duara na urefu wa kipenyo hadi tarakimu 7 nyuma ya nukta (3.1415926).

Katika kipindi cha enzi za kusini na kaskazini, uchumi ulikuzwa zaidi katika sehemu ya kusini, kwa kuwa watu walioishi sehemu ya kati walihamia sehemu ya kusini kwa kujiepusha na vita, hali ambayo si kama tu iliongeza nguvukazi ya sehemu ya kusini, bali pia ilihimiza sana maendeleo ya uchumi ya sehemu ya kusini kutokana na kuingia huko kwa teknolojia ya kisasa.

Katika kipindi hicho, maingiliano na nchi za nje yaliendelezwa kwa nguvu na kufikia hadi Japan, Korea kwa upande wa mashariki, Asia ya kati na Rome kwa upange wa magharibi na kufikia sehemu ya Asia ya kusini mashariki.

Ingawa maendeleo ya uchumi yalikwama katika enzi za sehemu ya kusini na enzi za sehemu ya kaskazini, lakini kutokana na utawala wa makabila yaliyotoka nje, makabila yaliyoko katika sehemu ya kati yaliungana pamoja,. Katika hali ya namna hiyo, makabila mengine yaliyotoka sehemu ya kaskazini yaliunganishwa na kabila la wahan na kuwa kabila moja. Hivyo, mfarakano wa enza za kusini na kaskazini ulifanya kazi muhimu ya kuunganisha makabila ya China, na ni moja ya sehemu muhimu ya maendeleo ya China.