Enzi za Sui na Tang
中国国际广播电台
Tangu Yang Jian ambaye alikuwa ni mfalme kuasisi enzi ya Sui mwaka 581, hadi Yang Guang ambaye alikuwa mfalme Yang aliponyongwa mwaka 618, enzi ya Sui ilidumu kwa miaka 37 tu. Mchango aliotoa mfalme Wen ulikuwa mkubwa zaidi ambao ni pamoja na kubatilisha utaratibu wa zamani wa enzi ya Zhou ya kaskazini, kubuni sheria mpya ambayo siyo yenye adhabu kali kama ya enzi ya Nanbei.

Tangu kuanzishwa enzi ya Tang mwaka 618 hadi enzi hiyo kuangushwa na Zhu Wen mwaka 907, enzi ya Tang ilidumu kwa miaka 289. Enzi ya Tang inagawanyika katika vipindi viwili kutokana na uasi wa Anshi. Katika kipindi cha kwanza enzi ya Tang ilistawi, na katika kipindi cha pili Tang ilizorota. Tanggaozu aliasisi enzi ya Tang, lakini Li Shimin ambaye alikuwa mfalme Tangtaizong aliongoza jeshi kuunganisha nchi nzima kwa kutumia miaka kumi. Baada ya kutokea uasi wa Xuanwumen, Li Shimin alikuwa mfalme, baada ya juhudi kubwa, enzi ya Tang ilistawi kuliko enzi zote za China, na iliongoza duniani katika siasa, uchumi na utamaduni. Lakini ilipofika kipindi cha mfalme Tangxuanzong licha ya kutokea hali ya ustawi vilevile ilianza kuzorota baada ya kutokea uasi wa Anshi.

Katika kipindi cha mwisho, siasa ya enzi ya Tang ilijaa ufisadi, uasi ulitokea huku na huku, hatimaye ulitokea uasi mkubwa wa Huang Chao, mmoja wa kiongozi aliyeongoza uasi huo Zhu Wen alijisalimisha kwa enzi ya Tang, na hapo baadaye alinyakua madaraka ya utawala wa enzi ya Tang na kuwa mfalme, aliasisi enzi ya Liang ya kipindi cha pili.