Enzi ya Song
中国国际广播电台
Mwaka 960, Zhao Kuangyin aliongoza uasi wa kijeshi na kuasisi utawala wa Song, ambao uliodumu kwa miaka 319 na uliangushwa na enzi ya Yuan mwaka 1279. Enzi ya Song ilipitia vipindi viwili vya Song ya kaskazini na Song ya kusini. Katika wakati huo huo, watu wa kabila la Qidan waliasisi nchi ya Liao ambayo ilidumu kuanzia mwaka 947 hadi mwaka 1125; Watu wa kabila la Dangxiang waliasisi nchi ya Xia ya magharibi (1038-1227) kwenye sehemu ya kaskazini magharibi ya enzi ya Song; Mwaka 1115 watu wa kabila la Nuzhen walianzisha nchi ya Jin (1115-1234) katika sehemu ya kaskazini. Mwaka 1125 nchi ya Jin ilimeza nchi ya Liao, na katika mwaka 1127 iliteka Kaifeng, mji mkuu wa enzi ya Song na kuwateka nyara wafalme wa Hui na Qin. Zhaogou wa enzi ya Song alichukua wadhifa wa ufalme katika Henan, hapo baada ye alitorokea Linan, ambayo hivi sasa inajulikana kwa Hangzhou iliyoko sehemu ya kusini, na kuasisi enzi ya Song ya kusini.

Enzi ya Song ya kaskazini baada ya kuunganisha sehemu za kaskazini, yalikuwa na maendeleo makubwa katika jamii, uchumi, utamaduni pamoja na biashara na nje baada ya nchi ya Jin kuangusha utawala wa Song ya kaskazini, Song ya kusini ilikalia sehemu ya kusini ambayo haikuwa na wazo la kushambulia sehemu ya kaskazini na kuunganisha upya sehemu ya kaskazini.

Katika kipindi hiki yalipatikana maendeleo makubwa katika sayansi na teknolojia hususan kuvumbua dira, teknolojia ya uchapishaji na baruti. Teknolojia iliyovumbuliwa na Bishen ya uchapishaji kwa kutumia chapa za neno moja moja ilitangulia kwa miaka 400 kuliko ile teknolojia ya Ulaya. Mbali na hayo, katika upande wa utamaduni walijitokeza wananadharia pamoja na kuenezwa kwa dini za kidao, kibudhaa pamoja na dini zilizotoka nchi za nje. Katika fasihi, walijitokeza waandishi wakubwa wa vitabu pamoja na maandishi na michoro mashuhuri.