Enzi ya Yuan
中国国际广播电台
Tiemuzhen wa Mongolia aliasisi nchi yake mwaka 1206, ambayo ilipewa jina la Yuan na mfalme Hubilie mwaka 1271. Enzi ya Yuan iliiangusha enzi ya Song mwaka 1279 na kuuchagua mji wa Daou, ambao ni Beijing kwa hivi sasa, kuwa mji mkuu wake.

Mwanzoni kabisa kabila la wamongolia lilikuwa katika sehemu ya kaskazini ya jangwa kubwa, Tiemuzhen alishinda makabila yote madogo madogo ya huko na kuazisha nchi ya Mongolia, naye akajiita kuwa mfalme Chengjisihan. Kabla ya hapo jeshi la Mongolia liliishambulia sehemu ya magharibi hadi Asia ya kati, Ulaya ya mashariki na Uajemi. Nchi hiyo kubwa, ambayo kitovu chake ni Jamhuri ya Watu wa Mongolia ya hivi sasa ilifarakana na kugawanyika kuwa nchi kadhaa za kifalme, ambazo kwa jina zilikuwa chini ya mfalme wa Chengjisihan.

Katika enzi ya Yuan, nchi zilizokuwa sehemu ya kaskazini zilipigana vita kwa miaka mingi na kuleta uharibifu mkubwa. Mfalme wa kwanza wa enzi ya Yuan aliweka kipaumbele katika kilimo na kurekebisha mto Manjano.

Katika enzi za Tang, Song na Yuan China ilikuwa nchi iliyoendelea kabisa duniani, ambayo uchumi na utamaduni vilivutia sana nchi jirani. Katika kipindi kile mabalozi, wafanyabiashara na wasomi wengi wa nchi za mashariki na magharibi walitembeleana, na uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na nchi za nje ulikuzwa kwa haraka. Nchi ya Yuan ilikuwa na uhusiano mkubwa na Japan pamoja na nchi za Asia ya kusini mashariki, na kwenye bahari merikebu (mashua kubwa) nyingi za China zilikuwa zikisafiri kati ya China na India. Uvumbuzi mkubwa tatu za uchapaji, baruti na dira zilienezwa hadi Ulaya kwa kupitia Uarabu katika enzi ya Yuan. Elimu ya sayari, tiba na hisabati ziliingia China na dini ya kiislamu ilienezwa katika China. Mawasiliano kati ya China na peninsula ya uarabuni licha ya kupitia baharini kulikuwa na njia ya kupitia mkoa wa Yunan kwenye nchi kavu, ambapo vyombo vya kauri vya China vilisafirishwa hadi Afrika ya mashariki hata nchini Morocco. Mwaka 1275, mtoto wa mfanyabiashara mashuhuri wa Venice alifuatana na babake walifika China na kuishi kwa miaka 17, kitabu walichoandika kijulikanacho kwa “kumbukumbu ya matembezi” kilikuwa kitabu muhimu kuhusu kuifahamu China na Asia kwa watu wa nchi za magharibi katika karne kadhaa.

Katika upande wa utamaduni, walijitokeza watungaji wa michezo ya opera wakiwa ni pamoja na Guan Hanqing, Wang Shipu, Bai Pu na Ma Zhiyuan.

Utawala wa Mongolia uliwakandamiza sana watu wa kabila la wahan, ambao ulisababisha upinzani mkubwa. Mwaka 1333, wakulima waliounganishwa kwa shughuli za kidini na jumuiya mbalimbali walifanya uasi sehemu mbalimbali nchini. Mwaka 1351 wakulima waliopelekwa kurekebisha mto Manjano walifanya uasi mkubwa wakijitambulisha kwa kufunga skafu nyekundu vichwani. Mwaka 1341 jeshi la “skafu nyekundu” liliangusha utawala wa Yuan na kuanzisha enzi ya Ming.