中国国际广播电台
Mwaka 1368 Zhu Yuanzhang alikuwa
mfalme katika mji wa Nanjing
na kuanzisha enzi ya Ming. Kwa
muda wa miaka 31 tangu awe mfalme,
mfalme Ming Taizu aliimarisha
madaraka ya udikteta wa kimwinyi,
kuua mawaziri wenye mafanikio
na wapinzani ili kuimarisha
utawala wake. Baada ya mfalme
Ming Taizu kufariki, mjukuu
wake Jianwen alirithi ufalme,
lakini alishindwa kwa jeshi
la baba yake mdogo. Tokea hapo
Zhuli akawa mfalme na kujiita
kuwa Ming Chengzu. Mwaka 1421
alihamishia mji mkuu mjini Beijing.
Ingawa enzi ya Ming iliimarisha
madaraka ya kifalme, lakini
wafalme wengi ama walikuwa
mbumbumbu au walikuwa bado
watoto na kutoshughulikia
mambo ya nchi, hivyo madaraka
yalitwaliwa na watumishi wa
jumba la mfalme, ambao walitamani
mali, kuwaua mawaziri adilifu
na kusababisha mgongano wa
kijamii. Ingawa wakulima walifanya
uasi mara kadhaa katikati
ya kipindi cha enzi ya Ming,
lakini wote walikandamizwa.
Katika enzi ya Ming alikuwepo
mwanasiasa mashuhuri Zhang
Juzheng, aliyefanya mageuzi
ili kupunguza mgongano wa
kijamii na kuimarisha nguvu
ya utawala wa enzi ya Ming.
Kilimo kilikuwa na maendeleo
makubwa zaidi katika enzi
ya Ming kuliko enzi za zamani,
ambapo sekta nyingine za nguo,
vyombo vya kauri, uchimbaji
wa madini ya chuma, utengenezaji
wa vyombo vya shaba, karatasi
na uundaji wa marikebu pia
vilipata maendeleo. Katika
enzi ya Ming uhusiano wa kiuchumi
na kiutamaduni ulikuzwa. Msafiri
mkubwa Zheng He alisafiri
mara 7 baharini hadi nchi
na sehemu zaidi ya 30 za Asia
na Afrika. Lakini baada ya
hapo, Enzi ya Ming ilivamiwa
na Japan, Hispania, Ureno
na Uholanzi.
Katika kipindi cha mwisho
cha enzi ya Ming, jamaa za
wafalme na majemedari walikuwa
na mashamba mengi, kodi za
serikali pia zilikuwa nyingi,
hali hiyo ilisababisha mgongano
mkubwa wa kijamii. Baadhi
ya maofisa walitarajia kupunguza
mgongano wa kijamii, wakidai
kudhibiti haki maalumu za
watumishi wa jumba la mfalme
na mabwenyenye, lakini walikandamizwa
na wenye madaraka, hali ambayo
ilizidisha hali ya wasiwasi.
Mwaka 1627 yalitokea maafa
ya makubwa ya kimaumbile,
lakini maofisa waliwalazimisha
wakulima kulipa kodi, jambo
ambalo lilisababisha wakulima
kufanya uasi. Mwaka 1644 jeshi
la wakulima liliuteka mji
wa Beijing, na mfalme Chongzhen
alijiua.
|