中国国际广播电台
Enzi ya Qing ilikuwepo kuanzia
mwaka 1644 hadi mwaka 1911,
muda ambao kulikuwa na wafalme
12 na kutawala China kwa miaka
268.
Enzi ya Qing ilipokuwa na
nguvu kubwa kabisa ilikuwa
na ardhi yenye eneo la kilomita
za mraba milioni zaidi ya
12. Mwaka 1616 Nuerhachi alianzisha
enzi ya Jin ya pili, mwaka
1636 mfalme Huangtaiji alibadilisha
jina la nchi kuwa Qing. Mwaka
1644 jeshi la wakulima lililoongozwa
na Li Zicheng liliangusha
enzi ya Ming, mfalme Chongzhen
wa enzi ya Ming alijiua. Jeshi
la Qing liliingia sehemu ya
kati ya China na kutumia nafasi
hiyo kulishinda jeshi la wakulima
na kuuchukua Beijing kuwa
mji mkuu wa Qing. Enzi ya
Qing ilivunjilia mbali majeshi
ya wakulima yaliyokuwa kwenye
sehemu mbalimbali za China
na kuunganisha sehemu zote
za China hatua kwa hatua.
Ili kupunguza mgongano wa
kijamii, mwanzoni enzi ya
Qing ilihamasisha wakulima
kufyeka mashamba na kutekeleza
sera za kupunguza kodi, hatua
hiyo iliyochukuliwa ilileta
maendeleo ya jamii na uchumi
kwenye sehemu za ndani na
mipakani. Ilipofika katikati
ya karne ya 18, uchumi wa
enzi ya Qing ulikuzwa zaidi
na kufika kileleni, nguvu
ya nchi ilikuwa kubwa, utaratibu
wa jamii ulikuwa shwari, na
idadi ya watu ilifikia kiasi
cha milioni 300.
Mwaka 1661 Zheng Chenggong
aliongoza kundi la manowari
kuvuka mlango bahari wa Taiwan
na kuwashambulia wakoloni
wa uholanzi waliokalia Taiwan
kwa miaka 38. Mwanzoni mwa
mwaka uliofuata, wakoloni
wa Uholanzi walisalimu amri,
na Taiwan ilirejea China.
Katika miaka ya mwisho ya
karne ya 16 Urusi ya Tsar
ilijipanua kwa sehemu ya mashariki.
Wakati jeshi la Qing lilipoingia
sehemu ya kati ya China, mfalme
Tsar wa Urusi alitumia nafasi
hiyo kukalia sehemu kadhaa
zikiwemo Yaksa na Nibuchu.
Serikali ya Qing ilitaka wavamizi
wa Urusi waondoke kutoka ardhi
ya China. Mwaka 1685 na mwaka
1686 mfalme Kangxi aliamuru
jeshi la Qing kushambulia
jeshi la mfalme Tsar wa Urusi
lililoko Yaksa, ambapo lililazimika
kukubali kutatua suala la
mpaka wa sehemu ya mashariki
kati ya China na Urusi kwa
njia ya mazungumzo. Mwaka
1689, wawakilishi wa China
na Urusi walikuwa na mazungumzo
huko Nibuchu na kusaini rasmi
“mkataba wa mpaka wa Nibuchu”.
Katika kipindi cha kati cha
enzi ya mfalme Qianlong, serikali
ilituliza kundi la wafarakanishaji
la Geerdan wa sehemu ya Zhungeer
na uasi uliofanywa na kabila
la wahui, kuunganisha sehemu
zote za Xinjiang na kutekeleza
sera kadhaa za kuhimiza uchumi,
utamaduni na mawasiliano ya
sehemu ya mpakani.
Kabla ya kipindi cha mfalme
Daoguang, enzi ya Qing ilipata
maendeleo makubwa katika mambo
ya utamaduni, ambapo walijitokeza
waandishi wakubwa wa vitabu
na vitabu vikubwa mashuhuri.
Vilevile maendeleo mengi katika
eneo la sayansi na teknolojia
hususan katika sekta ya ujenzi
wa majengo.
Mwaka 1840 vilizuka vita
vya kasumba, baada ya hapo
nchi za kibeberu ziliishambulia
China, ambapo utawala wa enzi
ya Qing ulisaini mikataba
mingi isiyo ya haki, kuzipa
ardhi, kutoa fidia na kufungua
milango ya miji ya pwani kwa
shughuli za biashara, Jamii
ya China ilibadilika hatua
kwa hatua kuwa nchi ya nusu
kimwinyi na nusu ya kikoloni.
Katika kipindi cha miaka ya
mwisho siasa ya enzi ya Qing
ilijaa ufisadi, kushikilia
wazo lile la kizamani, kuwa
waoga na unyonge na kuzorota
mwaka hadi mwaka. Watu wa
China waliishi kwa taabu kubwa
walianzisha harakati za kupinga
ubeberu na umwinyi. Ili kujiokoa
watawala walifanya baadhi
ya mageuzi wakijaribu kufanya
China kushika njia ya ustawi,
lakini hatimaye walishindwa
kabisa. Mashujaa wengi walipigana
vita kufa na kupona wakijitahidi
kuiokoa China. Mwaka 1911
yalitokea mapinduzi ya Xinhai
ambayo yaliuangusha utawala
wa enzi ya Qing na kumaliza
utaratibu wa kimwinyi uliodumu
kwa miaka zaidi ya 2,000,
tokea hapo China iliingia
katika kipindi kipya.
|