中国国际广播电台
“Kitabu
cha Historia” ni maandishi
makubwa ya historia ya China,
ni maandishi makubwa ya fasihi
ya kuandika watu na mambo
halisi, na kulikuwa na athari
kubwa kwa elimu ya historia
na fasihi kwa vizazi vilivyofuta
vya China. “Kitabu cha Historia”
kiliandikwa na Si Maqian katika
enzi ya Han ya magharibi,
karne ya kwanza kabla ya Kristu
kuhusu mambo yaliyotokea katika
miaka 3,000 iliyopita ya maeneo
ya siasa, uchumi, utamaduni
na historia tangu zamani za
kale hadi enzi ya Han ya magharibi.
Kitabu hicho alichoandika
Si Maqian kwa miaka 13, kina
makala 103 zenye maneno ya
kichina zaidi ya laki 5, mambo
aliyoandika ni pamoja na elimu
ya sayari, kalenda, miradi
ya maji, uchumi na utamaduni;
shughuli na mambo kuhusu koo
za kifalme na mabwenyenye
za enzi mbalimbali; na mambo
kuhusu watu mashuhuri wa enzi
mbalimbali na historia ya
makabila madogomadogo. “Kitabu
cha Historia” kiliandika mambo
halisi wala siyo kama vitabu
vitatu walivyoandika maofisa
wa historia wa enzi mbalimbali,
ambavyo viliandika mafanikio
tu na kusifu wafalme na mawaziri
wao.
|