Kuhusu Xu Fu Kwenda Japan
中国国际广播电台

 Baada a Qinshihuang kuwa mfalme wa enzi ya Qin, alitawaliwa na tamaa ya kuwa na maisha ya kudumu, alipata habari kuwa kuna mlima kwenye bahari ya Bo, ambapo kuna dawa zinazoweza kufanya mtu anayekula dawa hiyo kutofariki, hivyo alituma watu kwenda kutafuta dawa hiyo, lakini hawakuona dawa hiyo.

Lu Sheng alirudi na mikono mitupu, mfalme Qinshihuang akamtuma Xu Fu kwenda kuitafuta dawa hiyo tena. Xu Fu aliporudi kutoka baharini alimwambia mfalme kuwa aliona mlima wa Penglai na dawa hiyo pia, lakini viumbe waliokuwa wanaoishi kwenye mlima huo walimnyima na kusema kuwa zawadi aliyopeleka ni kidogo sana, na walisema kuwa mfalme akitaka dawa hiyo, sharti awapelekee wanaume, wanawake na mafundi hodari. Mfalme alifurahi sana baada a kusikia kuwa Xu Fu aliona dawa hiyo, akachagua watoto elfu 3 wa kike na wa kiume pamoja na mafundi hodari, alimtuma Xu Fu kwenda tena kwenye mlima wa huo. Xu Fu hakuona dawa hiyo, lakini aliogopa kurejea na kuonana na mfalme, hivyo aliongoza watu hao kwenda Japan na wakaanza kuishi huko. Hatimaye Xu Fu alifariki kwenye mlima wa Fuji nchini Japan.

Nchini Japan kuna hadithi na maandishi mengi ya kumbukumbu kuhusu Xu Fu, hata baadhi ya wanaelimu wanaona kuwa Xu Fu ndiye mwanzilishi wa nchi ya Japan, watu wa Japan vilevile wanamchukulia Xu Fu kama mtakatifu wa jadi na kumwabudu.