Uchimbaji wa Mapango ya Mogao
中国国际广播电台
Mapango ya Mogao ni ya kwanza kwa ukubwa na kamilifu ya mabaki ya dini ya kibudha duniani. Hiyo kama bohari ya vitu va sanaa inayofuatiliwa na watu wengi duniani, kwa nini ilijengwa kwenye genge la mlima ulioko kwenye jangwa la Gobi, sehemu ya kaskazini magharibi ya China?

Inasemekana kuwa mahali palipochimbwa mapango ya Mogao huko Denghuang palichaguliwa na mtawa Yue Zun. Mwaka 366 Yu Zun katika matembezi yake alifika chini ya mlima wa Sanwei, wakati ule ulishakuwa jioni, lakini hakupata mahali pa kulala, alipokuwa akiwaza, ghafla alinyanyua kichwa na kuona maajabu kwamba kulikuwa na mwangaza wa rangi ya dhahabu kwenye mlima uliotazamana naye, na kama kulikuwa na budha walioonekana katika mwangaza. Yue Zun alishangazwa sana na kuona kuwa kumbe hapo ni mahali patakafitu! Hivyo alitafuta watu kuchimba kwenye genge la mlima huo, na kulikuwa na mapango zaidi ya 1,000 ktika enzi ya Tang.

Utafiti uliofanywa na wataalamu unaonesha kuwa uchimbaji wa mapango ya mawe ya Mogao ni mafanikio ya akili ya mababu jadi, mapango kuchaguliwa kuchimbwa kwenye jangwa ni kutokana na wazo la kuungana na mazingira ya kimaumbile na kutengana kati ya dini ya kibudha ya maisha na desturi ya binadamu.