中国国际广播电台
Mwaka 1860 jeshi la mungano
la Uingereza na Ufaransa lilivamia
Beijing na kuingia bustani ya
Yuanming, walichukua kila kitu
chenye thamani. Vitu vya zawadi
lilivyotoa jeshi la Ufaransa
kwa mfalme wake baada ya kurejea
nchini vilikuwa karibu elfu
10. Hivi sasa watu wakitaka
kuona vitu vilivyokuwako katika
bustani ya Yuanming hawana budi
kwenda nchini Uingereza na Ufaransa.
Katika Jumba la Makungusho
la Uingereza mjini London
vinaoneshwa vitu vyenye thamani
elfu makumi kadhaa vilivyochukuliwa
kutoka bustani ya Yuanming.
Mfalme Napoleon wa tatu wa
Ufaransa alijenga ‘Jumba la
China” katika boma moja maarufu
la nchini Ufaransa kwa kuonesha
vitu zaidi ya elfu moja vya
utamaduni vya China.
|