Tetesi Kuhusu Visukusuku vya Sokwe-Mtu Wa Beijing
中国国际广播电台

 Visukuku vya sokwe-mtu wa Beijing kabla ya kupotea vilihifadhiwa katika sanduku la chuma la usalama la hospitali moja ya mji wa Beijing.

Siku chache kabla ya kuzuka vita ya Pasifiki, profesa Wei Dunrui, ambaye ni mtaalamu mashuhuri wa utafiti wa visukuku hivyo, aliona kuwa hospitali hiyo haikuwa mahali salama tena, hivyo alipendekeza kuvipeleka na kuhifadhiwa visukuku hivyo nchini Marekani. Siku moja ya wiki 2 au 3 kabla ya kuzuka tukio la Pearl Harbor, ofisa wa idara ya huduma ya hospitali hiyo Bo Wen aliarifu kuviweka visukuku 147 yakiwemo mafuvu 5 katika masanduku mawili ya mbao na kuyasafirisha hadi kwenye ubalozi wa Marekani mjini Beijing ili yasafirishwe pamoja na askari wa Marekani hadi Marekani. Lakini tokea hapo visukuku hivyo vilipotea na hakuna habari yoyote kuhusu visukuku hivyo.

Katika miaka ya karibuni, mtaalamu kuhusu elimu ya binadamu Bw. Zhou Guoxing alisikia kuwa siku chache kabla ya kusuka tukio la Pearl Harbor, askari mmoja aliyelinda mlango kati ya makao makuu ya jeshi la baharini la Marekani na ofisi ya ubalozi wa Marekani, aliona watu wawili walikuwa wakibeba sanduku moja na kulifukia katika ua ulioko sehemu ya nyuma ya nyumba ya ofisi ya ubalozi, na alikisia kuwa vitu vilivyokuwemo ndani ya sanduku hilo vilionekea kuwa ni visukuku vya sokwe-mtu wa Beijing. Bw. Zhou Guoxing alifika hapo, lakini hakuweza kuchimba, kwani sehemu hiyo imejengwa nyumba. Visukuku hivyo vilipotea kabla ya miaka miongo kadhaa iliyopita na hakuna habari yoyote kuhusu vitu hivyo. Hayati Zhou Enlai alipokuwa hai aliwahi kusema kuwa ni wachina kadhaa, ambao walikabidhi visukuku vya sokwe-mtu kwa wamarekani na vilipotea mikononi mwa wamarekani, wanasayansi waadilifu wangevirudisha kwa China.