中国国际广播电台
Kaburi la mfalme Qinshihuang
liko kwenye tarafa ya Yanzhai,
umbali wa kilomita 5 upande
wa mashariki wa mji mkuu wa
wilaya ya Lintong mkoani Shanxi.
Ukiangalia kutoka angani, kaburi
hilo linaonekana kama piramidi
kubwa. Eneo la kaburi hilo lina
kilomita za mraba 66.25, ambalo
ni kubwa kwa zaidi ya mara 2
kuliko eneo la mji wa Xian wa
hivi sasa.
Tangu aliporithi ufalme
alipokuwa na umri wa miaka
13, mfalme Qinshihuang alianza
kujijengea kaburi kwenye mlima
wa Li, baada ya kuunganisha
nchi nyingine 6, alikusanya
watu zaidi ya laki moja kutoka
sehemu mbalimbali kuendelea
kumjengea kaburi, ujenzi uliendelea
kwa miaka 37 hadi alipokufa
akiwa na umri wa miaka 50.
Kitabu cha historia kinasema
kuwa jumba la kuwekea maiti
ya mfalme Qinshihuang lilichimbwa
chini ya chemchemi na kuimarishwa
kwa maji ya madini ya shaba,
ndani yake viliwekwa vito
na vitu vingine vyenye thamani.
Ili kuzuia wezi kuingia ndani
ndani ya jumba la kaburi iliwekwa
upinde na mishale mingi, ambayo
inajirusha yenyewe wakati
inapoguswa. Pembeni mwa kaburi
ziliwekwa sanamu nyingi za
askari na farasi. Usanifu
wa kaburi ulizingatia kuonesha
madaraka na heshima ya mfalme
huyo.
Kutokana na “Kitabu cha Han”
na kitabu cha “Maelezo ya
Shuijing”, kaburi la mfalme
Qinshihuang lilitobolewa na
Xiang Yu mwaka 206 kabla ya
Kristu. Xiang Yu alipeleka
askari laki 3 na kusafirisha
vitu vilivyokuwemo ndani ya
kaburi kwa siku 30.
Lakini wako baadhi ya watu
wanaosema kuwa mwandishi maarufu
wa “Kitabu cha Historia” aliandika
makala maalumu kuhusu mfalme
Qinshihuang, lakini hakueleza
hata neno moja kuhusu kuharibiwa
kwa kaburi la mfale Qinshihuang,
lakini mwandishi wa kitabu
cha “Maelezo ya Shuijing”
aliandika maelezo kamili katika
miaka 600 hapo baadaye kuhusu
matukio hayo, ambayo yanatia
watu mashaka.
Baada ya mwaka 1949, watafiti
wa mabaki ya kale wa China
walifanya uchunguzi juu ya
kaburi la mfalme Qinshihuang,
hususan baada ya kugunduliwa
kwa sanamu ya askari na farasi.
Watafiti hao walitoboa matundu
zaidi ya 200, waligundua matundu
mawili yaliyochimbwa na wezi,
ambayo yalikuwa na kipenyo
cha sentimita 90 na urefu
wa kwenda chini kwa mita 9,
lakini matundu hayo mawili
yako kwenye umbali wa mita
250 kutoka sehemu ya katikati
ya kaburi, na wote hawakuingia
katika jumba lililoko chini
ya ardhi. Hivyo, maelezo yaliyoandikwa
na Li Daoyuan kuhusu Xiang
Yu kuchimba kaburi si ya kweli.
Inakisiwa kuwa vitu walivyochukua
akina Xiang Yu vilikuwa vitu
vilivyoko katika majengo mengine
ya kaburi la mfalme Qinshihuang.
Kama hali halisi ni kama ilivyokisiwa,
basi kaburi la mfalme Qinshihuang
litakuwa jumba la kwanza kwa
ukubwa duniani lililoko chini
ya ardhi.
|