 |
 |
 |
 |
 |
Habari kuhusu njia ya hariri |
 |
中国国际广播电台
Njia ya hariri ni njia muhimu
ya kuenea kwa ustaarabu wa kale
wa China kwa nchi za magharibi,
na ni daraja la maingiliano
ya uchumi na utamaduni kati
ya China na nchi za magharibi.
Njia ya hariri inaanzia mji
wa Changan kwa upande wa mashariki
hadi Rome kwa upande wa magharibi,
njia hiyo ina matawi mawili,
ambayo njia ya kusini omatpla
Denghuang kupitia Xinjiang na
Afghanistan, Iran, peninsula
ya Uarabu hadi nchi ya Rome.
Njia ya kaskazini inatoka Denghuang,
kupitia sehemu ya Asia ya kati
ya Russia kisha inaelekea upande
wa kusini magharibi na kuungana
na njia ya ile ya kusini. Njia
zote mbili zinajulikana kama
ni “njia za hariri ardhini”.
Aidha, kuna njia mbili za hariri
ambazo watu wengi hawazifahamu.
Moja ya njia hiyo inajulikana
kwa j9na la “njia ya hariri
ya kusini magharibi”. Njia hiyo
inatoka mkoa wa Sichuan, kupitia
mto wa Yiluowadi, Menggong iliyoko
sehemu ya kaskazini ya nchi
ya Myanmarr, baada ya kuvuka
mto wa Qindun, inafikia Nepal
iliyoko sehemu ya kaskaizni
mashariki ya India, kisha inafuata
mto wa Ganges, kisha inapitia
sehemu ya kaskazini magharibi
ya India na kufika kwenye uwanda
wa juu wa Iran. Njia hiyo ya
hariri ilikuweko mapema zaidi
kuliko zile za ardhini.
Njia nyingine ya hariri inatoaka
mji wa Guangzhou, kupitia mlango
bahari wa Malacca, Sri lanka,
India hadi Afrika ya mashariki.
Njia hiyo inajulikana kwa “njia
ya hariri ya baharini”. Mabaki
ya kale yaliyofukuliwa kutoka
baadhi ya sehemu za Afrika mashariki
ikiwemo Somalia, yanathibitisha
kuwa njia hiyo ya hariri ilianzishwa
katika enzi ya Song ya China.
“Njia ya hariri ya baharini”
iliunganisha nchi muhimu za
asili ya ustaarabu na sehemu
za chanzo cha utamaduni duniani,
ambazo zinahimiza maingiliano
ya uchumi na utamaduni ya katika
sehemu hizo, hivyo inaitawa
kuwa ni “njia ya mazungumzo
kati ya mashariki na magharibi.
Kitabu cha historia kinasema
kuwa msafiri Maco Polo hapo
zamani alifika China kwa kupitia
“Njia ya hariri ya baharini”.
Wakati aliporejea nyumbani pia
alipanda marikebu kutoka Quanzhou
ya mkoa wa Fujian na kuridi
Venice, Italia.
|
|
 |
|
|
 |
|
 |
 |
 |
 |
|
|
|
|