Kuhusu Majina ya Mahali Kisiwani Taiwan
中国国际广播电台
Katika historia, Taiwan iliwahi kuitwa kuwa Yizhou, Dongfan na Dayuan. Hapo baadaye watu waliita Taiwan kuwa “Kisiwa cha Hazina” kutokana na kuwa na rasilimali nyingi, “Kisiwa cha matufaha pori ya kichina” (umbo lake linafanana na majani yake), “Kisiwa cha Spring” (hali ya hewa yake si joto wala baridi), “Kisiwa cha Vipepeo” (kuna vipepeo wengi), kisiwa cha marijani (kuna marijani nyingi), na “Kisiwa cha Sukari” (kuna miwa mingi). Wakoloni wa Ulaya waliwahi kuita Taiwan kuwa “Farmosa” (Kisiwa Kizuri), vilevile waliwahi kuita Taiwan kuwa “Kisiwa cha Wavuvi”.