中国国际广播电台
Wachina wanaitwa kuwa “vizazi
vya dragon”, chanzo chake ni
alama na hadithi ya kale. Inasemekana
kuwa kabla ya mfalme Huang kulishinda
kabila la Ciyou na kuunganisha
sehemu za kati za China alichukulia
“dubu” kama ni alama yao, lakini
baada ya kuliteka kabila la
Ciyou ili kufariji maeneo yaliyojisalimisha
mfalme Huang aliacha kutumia
alama hiyo ya “dubu” na kutumia
“dragon” kama ni alama yao mpya,
ambayo ni mchanganiko wa kichwa
cha “dubu” na mwili wa aina
moja ya “nyoka”. Alama ya “dragon”
ni mchanganiko wa taswira za
jamii za wanaume na wanawake,
hali ambayo inaonesha historia
ya maendeleo ya taifa na mchakato
wa muungano wa makabila mbalimbali
ya China.
“Dragon” ikawa alama ya babu
za jadi za taifa la China,
hivyo taifa la China limehusishwa
na “dragon”. Kulikuwa na hadithi
inayosema kuwa mfalme Yan
ni mtoto wa mwanamke aliyejulikana
kwa jina la “Deng” kutokana
na kuhurumiwa na mungu wa
Dragon wa mbinguni. Maadamu
babu jadi wa taifa la China
alikuwa kizazi cha “Dragon”
wa mbinguni, hivyo vizazi
vya taifa la China vilevile
ni vizazi vya dragon.
|