Jinsi Utaalamu wa Ufunguji wa Mafunza wa Hariri Ulivyoenezwa Kwenye Nchi za Magharibi
中国国际广播电台
Inasemekana kuwa malkia Luo mke wa mfalme Huang aliwafundisha watu utaalam wa ufugaji wa mafunza wa hariri miaka zaidi ya 5,000 iliyopita.

Katika enzi ya Han ya magharibi, Zhang Qian alisafiri kwa upande wa magharibi na kupeleka vitambaa vya hariri hadi Ulaya. Watu wa Ulaya walipoona vitambaa laini na vya kung’ara walivinunua haraka.
Mwanzoni watu wa Ulaya hawakujua vitambaa hivyo vilifumwa kwa nyuzi zilizotolewa na mafunza wa hariri, walifikiri kuwa nyuzi hizo zilitolewa katika mti fulani, kisha kulainishwa kwa maji. Baada ya kujua kuwa vitamba hivyo vilifumwa kutokana na nyuzi za mafunza wa hariri, walipania kujifunza utaalam wa kufuga mafunza wa hariri.

 
Ilipofika karne ya 6, mfalme Jadincean wa Rome alionana na padri mmoja aliyewahi kufika China na kumtaka aende China kuiba mbinu ya kufuga mafunza wa hariri. Padri huyo alifika Yunnan, China alifahamishwa maarifa ya kufuga mafunza wa hariri kwa majani ya miforosadi, alirejea Rome kwa haraka, lakini alikanganyika badala ya kupasha joto mbegu wa mafunza kifuani mwake alizipanda kwenye ardhi na kuweka mbegu wa mti wa mforosadi kifuani mwake badala ya kuzipanda kwenye ardhi, hatimaye alishindwa. Padri huyo alituma mapadri wengine wawili waende China kukamilisha kazi hiyo, mapadri hao wawili walikumbuka sana fundisho alilopata yule padri wa kwanza na kuweka maandishi kuhusu upandaji miti na kupasha joto mbegu za mafunza wa hariri katika uwazi wa katikati ya bakora zao na kurudi Rome. Tokea hapo maarifa ya ufugaji wa mafunza wa hariri yaliingia barani Ulaya.