中国国际广播电台
Maneno ya kabila la wahan
ni moja ya maneno yaliyotumika
kwa miaka mingi, yenye nafasi
kubwa ya matumizi na kutumiwa
na idadi kubwa sana ya watu
duniani. Kuvumbuliwa na kutumika
kwa maneno ya kihan, si kama
tu kumehimiza maendeleo ya
utamaduni wa taifa la China
bali pia kumeathiri sana maendeleo
ya utamaduni wa dunia.
Zaidi ya miaka 6,000 iliyopita
kwenye sehemu yalipo majengo
ya Banpo, kulikuwa na aina
zaidi ya 50 za michoro, inayoonekana
kama ni maandishi ya kawaida,
wataalamu wanasema kuwa huenda
hiyo ndiyo asili ya maneno
ya kihan.
Maneno ya kihan yalikamilika
katika hatua ya mwanzo katika
enzi ya Shang karne ya 16
kabla ya Kristu. Katika kipindi
cha awali cha enzi ya Sahng,
ustaarabu wa China ulifikia
kiwango cha juu, na moja ya
alama yake ni kuwa na maandishi
yaliyochungwa kwenye magamba
ya kobe. Katika enzi ya Sahng,
mfalme kabla ya kufanya jambo
lolote alikuwa huagua, kwa
kutumia mabamba ya kobe.
Hivi sasa watafiti wa mabaki
ya kale wamegundua mabamba
ya kobe vipande zaidi ya elfu
160 vyenye maneno zaidi ya
4,000. Maandiko kwenye magamba
ya kobe yalikuwa msingi wa
maendeleo ya maneno ya kabila
la wahan.
Maandiko ya maneno ya kihan,
ambayo yanafanana na vitu
vyenyewe, yana maneno kiasi
cha elfu 10 na yale yanayotumika
mara kwa mara ni kiasi cha
elfu 3.
Kuvumbuliwa maneno ya kihan
kulileta athari kubwa kwa
nchi jirani. Maandiko ya kijapan,
kivietnam na kikorea yalivumbuliwa
kwa msingi wa maneno ya kihan.
|