Maajabu Yaliyogunduliwa kwa “Remote Sensing”
中国国际广播电台
Katika miaka ya karibuni wataalamu walipiga picha ya mji wa Beijing kutoka angani kwa teknolojia ya “remote sensing”, waliwaona dragon wawili waliolala na jitu mmoja lililo keti kwenye eneo la mji, hayo yamekuwa maajabu mawili ya mji wa Beijing.

Picha ya rangi iliyotokana na teknolojia hiyo inaonesha kuwa dragon wa kwanza anaundwa na majengo ya kale ya Beijing kuanzia jengo la Tiananmen hadi jengo la Zhonggu. Na dragon mwingine anaundwa na mito na mifereji ya Beijing na kujulikana kwa “dragon wa maji”.

Ajabu lingine la Beijing ni taswira ya bustani ya Jingshan ambayo inaonekana kama jitu moja lililokaa chini. Bustani ya Jingshan ilikuwa ya wafalme na iko katika upande wa kaskazini mwa majumba ya wafalme wa zamani. Je hali hiyo ni inatokana na kusanifiwa au ilitokea kwa bahati tu? Hilo ni swali ambalo mpaka sasa halijajibiwa.