中国国际广播电台
Katika kipindi cha zama mawe
cha zamani kiasi cha miaka elfu
50 iliyopita, binadamu walijua
kutengeneza na kutumia sindano.
Sindano hiyo ilitengenezwa kwa
mfupa. Watafiti waliwahi kugundua
sindano ya mfupa huko Ozuina
barani Ulaya, lakini sindano
ile ilitengenezwa kwa ufundi
wa kiwango cha chini sana. Sindano
iliyogunduliwa katika pango
waliloishi sokwe-mtu ilitengenezwa
kwa ufundi mkubwa zaidi.
Sindano hiyo ina urefu wa
milimita 82 na unene wa milimita
3, ambayo inafanana na njiti
ya kiberiti, sindano hiyo
ni laini na yenye ncha kali.
Watafiti wanasema kuwa sindano
hiyo inatufahamisha kuwa,
wahenga walioishi mapangoni
walikuwa wanavaa nguo.
Wahenga hao walikuwa wanaishi
kwenye mapango milimani miaka
zaidi ya elfu 18 iliyopita,
walijua kutengeneza na kuvaa
vitu vya mapambo. Watafiti
waligundua mkufu uliotengenezwa
kwa mawe, meno ya wanyama,
mfupa wa samaki na simbi za
baharini.
|