Mwandishi Su Shi
中国国际广播电台

      
Su Shi alizaliwa mwaka 1037 na kufa mwaka 1101, alikuwa mwenyeji wa Mkoa Sichuan. Baba yake alikuwa mwanafasihi, kuokana na kuathiriwa na baba yake, toka alipokuwa mtoto alikuwa na ari ya kupigania mustakbali mzuri wa maisha yake. Baada ya yeye kushika wadhifa alikuwa mtetezi wa kufanya mageuzi ili alitawale taifa kwa amani. Alipokuwa ofisa wa kisehemu na diwani wa mfalme alikuwa mwanamageuzi mwenye juhudi akijaribu kuondoa sera zenye madhara na kutetea zile zenye maendeleo.

Kutokana na tabia yake ya kudhihirisha wazi kila kitu moyoni mwake na kuthubutu kusema kinaganaga mbele ya mfalme, mwishowe alikuwa msingiziwa katika mivutano kati ya vikundi vya madiwani wa mfalme. Mara kadhaa alipewa adhabu ya kufukuziwa mbali, na kila mara mazingira ya kuishi yalikuwa mabaya zaidi. Kutokana na ugumu wa maisha alikuwa amepata falsafa ya Confucius, ya dini ya Buddha na ya dini ya Dao akawa mtu mwenye moyo mpana wa kujiliwaza kutokana na maisha yake magumu na huku alikuwa mtu mwenye matumaini mema ya binadamu na kuyapigania katika maisha yake.

Hulka ya Su Shi ya unyoofu bila kuficha lolote moyoni ilisifiwa sana katika kipindi cha mwisho cha jamii ya umwinyi nchini China na iliathiri wasomi kwa miaka 800.