中国国际广播电台
Katika
historia ya fasihi ya China
watu hutaja washairi wawili
wakubwa Li Bai na Du Fu kuwa
ni wawakilishi wa mafanikio
makubwa ya uashairi katika
Enzi ya Tang (618-907).
Du Fu alizaliwa mwaka 712,
alikuwa ni mjukuu wa mshairi
mashuhuri Du Shenyan. Du Fu
alikuwa mtoto mwenye kipaji
kisicho cha kawaida. Toka
utotoni mwake alikuwa na hamu
ya kujifunza na alipokuwa
na umri wa miaka 7 alianza
kutunga mashairi. Baada ya
kuwa mtu mzima alikuwa hodari
wa kuchora picha, kupanda
farasi na kucheza kitara.
Tokea alipokuwa na umri wa
miaka 19 alianza kutembelea
huku na huko kwenye mandhari
nzuri ya mito na milima na
alipata kuona mengi, wakati
huo kilikuwa ni kipindi cha
ustawi kabisa cha Enzi ya
Tang.
Kama walivyokuwa wasomi
wengi wengine wa China, Du
Fu pia alitamani kuwa na wadhifa
fulani katika utawala wa kifalme,
mara nyingi alikuwa anawasifu
watu wenye madaraka na matajiri
lakini hakupata chochote.
Alipokuwa mtu wa makamo aliishi
maisha ya kimaskini katika
mji mkuu wa Enzi ya Tang,
Chang An, na alishuhudia hali
ya kusikitisha ya watu maskini
kufa kwa njaa na baridi huku
matajiri wakiishi maisha ya
anasa, aliandika kifungu kinachojulikana
kwa wote hadi leo, “Nyama
na pombe zaoza nyumbani kwa
matajiri, watu maskini wanakufa
mitaani”. Maisha yake magumu
yalimfanya aelewe kwa kina
ufisadi wa watawala na janga
la watu maskini, na kumfanya
awe mshairi anayehangaikia
sana hali ya taifa na wananchi.
Mwaka 755 Du Fu alipokuwa
na umri wa miaka 43 alipata
wadhifa, lakini baada ya mwezi
mmoja vita vilizuka na kuendelea
kwa muda mrefu. Katika kipindi
hiki Du Fu alizurura zurura
akiwa na maisha magumu na
alikuwa ametambua vema jamii
aliyoishi na aliandika mashairi
mengi maarufu.
Mwaka 759 alikuwa amekata
tamaa kabisa kuhusu siasa,
aliacha wadhifa wake. Wakati
huo kulitokea ukame na maisha
yake yalikuwa ya kimaskini
kabisa na hata alishindwa
kuendelea na maisha yake,
aliwaongoza jamaa yake kwenda
kwenye mji uliopo katika sehemu
ya kusini magharibi ya China.
Kutokana na msaawa wa marafiki
zake aliishi kwa miaka minne
bila kuwasiliana na wengine,
wakati huo aliandika shairi
maarufu la kuelezea maisha
yake magumu la “Nyumba Iliyoezeuliwa
paa na Upepo”, akionesha matumaini
yake ya kukubali kulala mitaani
kama angeweza kuwapatia watu
wote nyumba ili wajihifadhi
kwenye ya kuhifadhi kwenye
joto.
Du Fu alifariki mwaka 770
alipokuwa na umri wa miaka
59 kutokana na umaskini na
ugonjwa akiwa katika safari
ya kuzurura. Mashairi ya Du
Fu yaliyobaki sasa yako 1400,
kwa kina yameonesha miaka
20 hali ya jamii yenye vurugu
ya vita, kutoka ustawi hadi
kuporomoka kwa uchumi katika
Enzi ya Tang.
|