中国国际广播电台
Li
Bai alizaliwa mwaka 701 na
kufariki dunia mwaka 762,
alikuwa mwenyeji wa mkoa wa
Gansu wa leo. Hadi sasa haijafahamika
kama alizaliwa katika ukoo
gani, lakini kutokana na mashairi
yake tunaweza kufahamu kuwa
yeye alizaliwa katika ukoo
wenye hali nzuri kiuchumi
na kiutamaduni. Tokea alipokuwa
mtoto alipenda kusoma na alisoma
vitabu vingi. Tangu alipokuwa
na miaka 20 alianza kutembelea
kila mahali ili kuona mengi.
Kutokana na elimu yake kubwa
na akili yake timamu, alifanikiwa
sana katika uandishi wa mashairi.
Ingawa wakati huo hali ya
uchapaji na mawasiliano ilikuwa
duni, lakini kupitia maingiliano
ya wasomi jina lake lilijulikana
sana.
Kusoma ili kujipatia nyadhifa
ni tumaini la wasomi wote
katika enzi za kale za China.
Li Bai alipokuwa kijana alikuwa
na tumaini kubwa la kupata
wadhifa, kutokana na lengo
hilo alikwenda mji mkuu wa
Enzi ya Tang, Changan. Kutokana
umaarufu wake na kupendekezwa
na wasomi, mwaka 742 alichaguliwa
kuwa afisa katika kasri la
mfalme. Huu ulikuwa ni wakati
mzuri kabisa maishani mwake.
Li Bai alikuwa ni mtu mwenye
kiburi, alikuwa na malalamiko
mengi kuhusu ufisadi na alitamani
kuthaminiwa zaidi na mfalme,
ili aoneshe uhodari wake katika
mambo ya siasa, lakini mfalme
alimchukulia kama ni mshairi
aliyetumiwa tu wakati mfalme
anapokuwa na haja naye. Li
Bai alikata tamaa, na aliondoka
mji mkuu Changan na kuanza
tena maisha ya kutembea tembea
kila mahali akiwa anajifariji
kwa kunywa pombe na kuandika
mashairi.
Mashairi ya Li Bai yaliyobaki
hadi sasa ni zaidi ya 900.
|