Mshairi wa kueleza mandhari ya maumbile Tao Yuanming
中国国际广播电台

      
Tao Yuanming pia anaitwa Tao Qian, alikuwa ni mshairi wa kueleza mandhari ya maumbile. Alikuwa mtu wa kuridhika na maisha yake ya umaskini, mwenye hulka ya unyoofu, wasomi wa baadaye walimsifu sana.

Baba wa babu wa Yuan Mingyuan alikuwa ni mwanzilishi wa Enzi ya Jin Mashariki, babu yake na baba yake wote walikuwa ni maofisa. Tao Yuanming alipokuwa na umri wa miaka minane baba yake alifariki, hali ya familia ikawa duni. Alipokuwa mtoto alikuwa na tumaini kubwa la kuwa ofisa na kutoa mchango katika mambo ya kisiasa.

Lakini Enzi ya Jin Mashariki kilikuwa ni kipindi cha vurugu, migogoro kati ya maofisa na ufisadi vilikithiri katika kasri la mfalme. Ilikuwa muda mfupi baada ya Tao Yuanming kuwa na wadhifa alipokuwa na umri wa miaka 29, alijiachisha kazi na kurudi nyumbani kutokana na kutoweza kuvumilia ufisadi huo.

Maisha ya Tao Yuanming yalikuwa mabaya siku hadi siku, na hata alishindwa kuwalisha jamaa zake kwa kulima, ilimpasa ajitafutie wadhifa, na alipokuwa na umri wa miaka 41 alikuwa ofisa wa wilaya. Lakini kutokana na hulka yake ya kuchukia matajiri na kujinyenyekea, alikuwa madarakani kwa siku 80 tu alijiachisha kazi. Tokea hapo alikuwa ameacha kabisa wadhifa na kuishi kwa kutegemea kilimo.

Maisha yake ya kilimo yalikuwa mabaya sana, alipokuwa na umri wa miaka 44 nyumba yake iliungua, maisha yalikuwa magumu zaidi. “Kukaa na njaa katika siku za joto, na kulala bila mfarishi katika siku za baridi” ni beti iliyoeleza hasa umaskini kwenye maisha yake. Lakini alikuwa na moyo mtulivu kuvumilia umaskini huo. Katika kipindi hicho aliandika mashairi mengi ya kueleza mandhari ya vijijini. Kutokana na kalamu yake, kwa mara ya kwanza maisha ya wakulima na mandhari ya vijijini ilikuwa mada muhimu katika maandishi.

Maisha ya uzeeni ya Tao Yuanming yalikuwa ya kusikitisha sana, hata mara nyingne alikuwa anaomba, hata hivyo alipokuwa maskini sana alikataa wadhifa kwa mara nyingine tena. Insha aliyoandika uzeeni “Matembezi katika Kijiji cha Taohuayuan” inajulikana kwa wote. Katika makala hiyo alieleza mvuvi mmoja aliyepotea njia aliingia katika kijiji hicho aligundua baadhi ya watu wanaoishi katika kijiji hicho, watu ambao kizazi kwa kizazi waliishi huko kwa ajili ya kukwepa vurugu za vita, walikuwa hawajui dunia ilivyo nje ya kijiji hicho, wote walikuwa ni watu wenye juhudi za kazi na waaminifu, wakiishi maisha ya utulivu bila wasiwasi. Maisha ya watu katika kijiji cha Taohuayuan yaliwakilisha matumaini mema ya mshairi Tao Yuanming ya amani badala ya jamii iliyojaa vurugu za vita.

Mashairi na makala za Tao Yuanmin zilizobaki ziko zaidi ya mia moja tu, lakini nafasi ya mshairi huyo katika historia ya fasihi ya Kichina ni muhimu sana.