中国国际广播电台
Qu Yuan ni mshairi anayependwa
na kuheshimiwa sana na Wachina.
Mshairi huyo aliishi katika
Kipindi cha Madola Yaliyopigana
Vita (475 K.K.—221 K.K.). Katika
kipindi hicho madola madogo
madogo yalikuwa mengi, na yalipigana
vita miaka hadi miaka. Kati
ya madola hayo, Dola la Qin
na Chu yalikuwa na nguvu zaidi,
madola mengine yalikuwa yakifuata
madola hayo mawili.
Qu Yuan alikuwa mtu wa tabaka
la matajiri na alikuwa ofisa
mwandamizi katika serikali.
Alikuwa mwenye elimu nyingi
na alikuwa hodari wa mambo
ya diplomasia, kwa hiyo alipendwa
na kuaminiwa sana na mfalme
wa Dola la Chu. Katika kipindi
hicho kila mfalme alikuwa
anawakusanya watu wenye elimu
kwa unyekekevu, na hali hiyo
ilishamiri sana katika kila
dola. Wasomi wengi wakubwa
walitembeatembea kati ya madola
ili watimize malengo yao ya
kisiasa. Lakini Qu Yuan alikuwa
kinyume na hali hiyo, aling’ang’ania
kukaa nchini Chu akitumai
kumsaidia mfalme wake kwa
elimu yake na kumwelimisha
mfalme awe fikra za kimaendeleo
na kulifanya Dola la Chu liwe
la nguvu na ustawi. Lakini
bahati mbaya aligongana sana
na kundi la matajiri katika
mambo ya ndani na nje, na
zaidi ya hayo alisingiziwa
na wengine, hivyo alipuuzwa
na mfalme wa Chu. Tokea hapo
hadhi ya Dola la Chu ilishuka
na nguvu zilififia. Mwaka
278 K.K. jeshi la Dola la
Qin lilivamia Dola la Chu
na liliteka mji mkuu wa Dola
la Chu. Taifa liliporomoka,
na Qu Yuan alijitumbukiza
mtoni kutokana na huzuni na
hasira.
Maandishi aliyowaachia watu
wa baadaye ni utenzi wake
Li Sao (uchungu wa moyo).
Utenzi huu kwa kutumia mifano
ya mambo ya kale alitamani
mfalme wa Chu angekuwa kama
wafalme werevu wa kale Yao,
Shun na Yu waliothamani watu
wenye elimu na hekima, na
kwa uadilifu na maadili kuendesha
utawala na kuunganisha madola
mengine kupambana na Dola
la Qin.
|