Kitabu cha Kwanza cha Mkusanyiko wa Mashairi
“Mashairi ya Kale”
中国国际广播电台


Katika karne ya saba K.K. kitabu cha kwanza kabisa cha mkusanyiko wa mashairi “Mashairi ya Kale” kiliandikwa. Ndani ya kitabu hicho yalikusanywa mashairi ya aina mbalimbali ya masimulizi ya matukio, mapenzi, vita na nyimbo za kusifu mambo fulani. Mashairi hayo hayakuandikwa na mtu mmoja. Kitabu hicho kilikusanya mashairi 305 yaliyokuwa katika miaka mia tano.

Mashairi katika kitabu hicho hapo awali yalikuwa kwa ajili ya matumizi ya kuimbwa katika sherehe, burudani na kuonesha fikra za kisiasa, na baadaye yalikuwa masomo ya watu wa tabaka la matajiri. Kusoma kitabu hicho kulikuwa dalili ya elimu ya juu. Masomo hayo yalisaidia sana lugha katika maingiliano ya kijamii, watu walikuwa wakitumia beti fulani za mashairi kueleza maana yake bila kusema moja kwa moja. Confucius aliwahi kusema, “bila kusoma ‘Mashairi ya Kale’ mtu hawezi kuongea”, alisifu sana kitabu hicho.

Kwa muhtasari, “Mashairi ya Kale” ni mwanzo wa fasihi kubwa ya China, ni dalili ya ustawi wa fasihi. Mashairi yake yalihusika na pande mbalimbali, na lugha yake ni tegemeo muhimu katika utafiti wa lugha ya Kichina katika kipindi cha karne ya 11 K.K. hadi karne ya sita K.K.