中国国际广播电台
Katika historia
ya fasihi ya milenia kadhaa,
walitokea washairi na waandishi
wengi wa tamthilia na riwaya,
Bw. Li Yu alikuwa mmojawapo.
Li Yu alizaliwa mwaka 1610
katika Enzi ya Ming. Katika
miaka alipokuwa na umri wa
miaka 30 ndipo mabadiliko
ya enzi za kifalme yalipotokea.
Enzi ya Qing ambayo ni enzi
ya mwisho ya umwinyi nchini
China iliiangamiza Enzi ya
Ming, na kusababisha msukosuko
wa jamii, msukosuko huo uliendelea
kwa miongo kadhaa. Maisha
ya Li Yu yalikuwa katika mazingira
hayo hadi alipokufa mwaka
1680.
Li Yu alifundishwa na fikra
za Confucius toka alipokuwa
mtoto akitamani kufuata njia
iliyochukuliwa na wasomi wengi
wa zamani yaani kupata wadhifa
kwa kufanikiwa katika mtihani.
Lakini bahati mbaya alikutana
na mazingira ya wasiwasi wa
jamii, alishiriki kwenye mtihani
mara kadhaa lakini mara zote
alishindwa. Tokea hapo aliacha
kabisa njia hiyo, alianzisha
duka ili alijipatie kipato
kwa kuwasaidia wengine kuandika
makala, na akiwa na muda alitunga
tamthilia.
Mafanikio makubwa maishani
mwa Li Yu ni tamthilia na
nadharia ya utungaji wa tamthilia.
Maandishi ya tamthilia yaliyobaki
ni kumi ikiwa ni pamoja na
“Samaki Wayo” na “Mapenzi
ya Phoenix”. Tamthilia zake
zote ni za kueleza mapenzi
na kusifu matumaini ya wapenzi
vijana, na kuponda mila ya
ndoa iliyoamuliwa na wazazi.
Tamthilia zake zinapendwa
sana na watazamaji na hata
ziliigwa katika nchi za kusini
mashariki za Asia, hadi sasa
tamthilia zake zinaendelea
kuigizwa.
Li Yu licha ya kuwa mwandishi
wa tamthilia, yeye pia ni
mwananadharia wa utungaji
tamthilia na mwandishi wa
riwaya. Riwaya zake za “Tamthilia
Isiyo na Sauti” na “Jumba
la Ghorofa” zinajulikana sana.
Katika riwaya zake alitetea
usawa kati ya wanaume na wanawake.
Katika historia ya fasihi ya
milenia kadhaa, walitokea washairi
na waandishi wengi wa tamthilia
na riwaya, Bw. Li Yu alikuwa
mmojawapo.
Li Yu alizaliwa mwaka 1610
katika Enzi ya Ming. Katika
miaka alipokuwa na umri wa
miaka 30 ndipo mabadiliko
ya enzi za kifalme yalipotokea.
Enzi ya Qing ambayo ni enzi
ya mwisho ya umwinyi nchini
China iliiangamiza Enzi ya
Ming, na kusababisha msukosuko
wa jamii, msukosuko huo uliendelea
kwa miongo kadhaa. Maisha
ya Li Yu yalikuwa katika mazingira
hayo hadi alipokufa mwaka
1680.
Li Yu alifundishwa na fikra
za Confucius toka alipokuwa
mtoto akitamani kufuata njia
iliyochukuliwa na wasomi wengi
wa zamani yaani kupata wadhifa
kwa kufanikiwa katika mtihani.
Lakini bahati mbaya alikutana
na mazingira ya wasiwasi wa
jamii, alishiriki kwenye mtihani
mara kadhaa lakini mara zote
alishindwa. Tokea hapo aliacha
kabisa njia hiyo, alianzisha
duka ili alijipatie kipato
kwa kuwasaidia wengine kuandika
makala, na akiwa na muda alitunga
tamthilia.
Mafanikio makubwa maishani
mwa Li Yu ni tamthilia na
nadharia ya utungaji wa tamthilia.
Maandishi ya tamthilia yaliyobaki
ni kumi ikiwa ni pamoja na
“Samaki Wayo” na “Mapenzi
ya Phoenix”. Tamthilia zake
zote ni za kueleza mapenzi
na kusifu matumaini ya wapenzi
vijana, na kuponda mila ya
ndoa iliyoamuliwa na wazazi.
Tamthilia zake zinapendwa
sana na watazamaji na hata
ziliigwa katika nchi za kusini
mashariki za Asia, hadi sasa
tamthilia zake zinaendelea
kuigizwa.
Li Yu licha ya kuwa mwandishi
wa tamthilia, yeye pia ni
mwananadharia wa utungaji
tamthilia na mwandishi wa
riwaya. Riwaya zake za “Tamthilia
Isiyo na Sauti” na “Jumba
la Ghorofa” zinajulikana sana.
Katika riwaya zake alitetea
usawa kati ya wanaume na wanawake.
|