中国国际广播电台
"Safari ya Kwenda Magharibi"
ni riwaya nzuri katika historia
ya fasihi ya kale ya China.
Riwaya hii ilitungwa kwa mujibu
wa vituko vilivyomkuta sufii
wa dini ya Kibuddha, Tang Zeng
(Tang Xuanzang), alipokuwa katika
safari yake ya kwenda India
kuchukua msahafu katika karne
ya 7 K.K. Katika riwaya hiyo
Wu Chengen alibuni wafuasi watatu
kufuatana na sufii huyo. Mmoja
wa wafuasi wake alikuwa mfalme
kima Sun Wukong. Sun Wukong
alikuwa na nguvu za kudura ya
mungu, anaweza kujigeuza sura
72 na fimbo yake ya kupambana
na mashetani yaweza kurefushwa
kuwa ndefu hadi mbinguni na
kufupishwa kuwa ndogo hadi kama
sindano ya kutia sikioni. Mfalme
kima Sun Wukong ndiye aliyeonesha
matumaini ya mwandishi kwamba
mambo yote maovu yatatokomezwa
kabisa katika jamii.
Wu Chengen ni mwenyeji wa
wilaya ya Huai An mkoani Jiangsu.
Tangu alipokuwa mtoto alikuwa
mwerevu na mshabiki wa mambo
mengi. Alikuwa hodari wa kuchora
picha, usanii wa maandiko
ya Kichina kwa brashi ya wino,
pia alipenda kukusanya na
kuhifadhi picha na maandiko
ya watu mashuhuri. Alipokuwa
kijana jina lake lilikuwa
maarufu sana katika sehemu
ya makazi yake kwa sababu
ya kipaji chake cha fasihi.
Lakini mara nyingi alishindwa
katika mitihani ya kifalme
ya kuchagua maafisa, na maisha
yake yakawa ya shida. Kutokana
na hayo akagundua ubovu ulioenea
miongoni mwa maafisa na jinsi
jamii ilivyotatanika, akawa
na kinyongo moyoni mwake.
Katika shairi lake moja alisema
kwamba ubovu wa jamii unatokana
na mfalme kuwatumia maafisa
wabovu. Alitaka kubadilisha
hali hiyo lakini hakuweza
kufanya lolote ila kuipigia
kite. Hivyo aliweka matumaini
na kinyongo chake kwenye riwaya
yake ya "Safari ya Kwenda
Magharibi".
"Safari ya Kwenda Magharibi"
iliandikwa na Wu Chengen katika
miaka yake ya uzeeni, lakini
matayarisho ya riwaya hiyo
yalimtumia maisha yake yote.
Alipokuwa mtoto mara kwa mara
alifuatana na baba yake kwenda
kwenye misitu minene na mahekalu,
na baba yake humweleza hadithi
za ajabu zilizotokea huko.
Hamu yake ya kusikiliza hadithi
utotoni mwake haikupungua
hata baada ya yeye kuwa mzima.
Baada ya kutimiza miaka 30
alikuwa amekusanya hadithi
nyingi za ajabu akanuia kuandika
riwaya. Alipofikia umri wa
miaka 50 hivi alikuwa amemaliza
sura 10 za mwanzo za riwaya
yake ya "Safari ya Kwenda
Magharibi", lakini baadaye
kwa sababu fulani aliacha
kwa miaka mingi hadi baada
ya kujiuzulu kazi na kuwa
nyumbani.
"Safari ya Kwenda Magharibi"
iliandikwa hadithi moja moja
lakini kila hadithi pia ni
sehemu ya riwaya nzima. Ndani
ya riwaya hiyo walitokea mashetani
na miungu mingi ambao wanawakilisha
haki na uovu. Kasri ya mbinguni
ilionekana adhama sana lakini
kwa kweli mungu aliyekuweko
ndani ya kasri hiyo alikuwa
mbabaishaji wa watu wema na
wabaya, akilenga mfalme duniani;
na kasri ya dunia ya pili
ingawa ilionekana ukakamavu,
lakini maofisa wanasaidiana
katika hatia, walikuwa hawajali
sheria na wadhulumiwa hawakuweza
kupata haki. Hayo alilenga
katika hali ya utawala wa
kifalme. Mashetani walikula
na kuwaua watu huku wakiwa
wachoyo wa mali na kupenda
warembo na kufanya uovu watakavyo.
Katika hayo mwandishi alifananisha
madhalimu na maofisa wa kifalme.
Kwa upande mwingine Wu Chengen
alifanikiwa kusawiri shujaa
kima Sun Wukong, ambaye alikuwa
mtetezi wa haki, alikuwa na
nguvu za kudura ya mungu na
mwenye msimamo bayana kati
ya watu wema na wabaya, fimbo
yake ina nguvu za ajabu. Hii
inaonesha tarajio la Wu Chengen
la kukomesha maovu yote katika
jamii aliyoishi.
Riwaya ya "Safari ya
Kwenda Magharibi" inajulikana
sana kwa wote wa China kutoka
kizazi hadi kizazi na katika
miaka mia kadhaa iliyopita
riwaya hii ni kama chimbuko
la kutunga hadithi kwa watoto
na michezo ya filamu na televisheni.
|