"Ndoto katika Jumba Jekundu"
中国国际广播电台

Katikati ya karne ya 18, kilikuwa ni kipindi cha ustawi mkubwa katika Enzi ya Qing, lakini katika kipindi hicho ilitokea riwaya ndefu iliyoashiria mporomoko utakaotokea katika jamii ya kimwinyi, riwaya hiyo ni “Ndoto katika Jumba Jekundu”.

"Ndoto katika Jumba Jekundu" ni riwaya iliyoandikwa na Cao Xueqin ambaye aliishi kati ya mwaka 1715 hadi 1763. Hapo mwanzo riwaya hiyo ilienea katika jamii kwa kunukuu kutoka wasomaji hadi wengine, kwa sababu riwaya hiyo ilishukiwa kuwa ililenga utawala wa wakati huo, kitabu chake cha kuchapwa rasmi lilikuwa ni jambo la baadaye. Mwandishi wa riwaya hiyo alizaliwa katika ukoo wa maofisa uliokuwa ukiporomoka kizazi hadi kizazi. Babu na baba wa mwandishi huyo wote walikuwa ni maofisa wakubwa katika utawala wa kifalme na walikuwa na uhusiano wa karibu na ukoo wa kifalme, lakini hadi miaka wakati ukoo wa mwandishi huyo ulipoporomoka kwa madaraka na hadhi, hata maisha yalikuwa magumu. Wengi wanaona kuwa Cao Xueqin aliandika riwaya hiyo kwa mujibu wa hali ya ukoo wake ilivyokuwa, na kutokana na umaskini mwandishi Cao Xueqin alifariki kabla kumaliza riwayake. Kitabu hicho kilipoenea kutokana na kunukuu alikuwapo mwandishi aliyeitwa Gao E, huyo ndiye aliyemmalizia riwaya yake na kuifanya riwaya hiyo kuwa na sura 120 za sasa.

Riwaya hiyo imeeleza jinsi jamii ya wakati ule ilivyokuwa kupitia maelezo kuhusu koo nne kubwa za "Jia, Shi, Wang na Xue", hasa maelezo kuhusu jinsi ukoo wa Jia ulivyostawi na kuporomoka. Uhodari mkubwa katika riwaya hiyo ni kueleza maisha halisi yalivyokuwa na sura halisi za wahusika walivyo. Ndani ya riwaya hiyo wahusika wafikia zaidi ya 400 na kila mmoja ana tabia na hulka yake mwenyewe, hakuna aliyefanana na mwingine, ikionesha ustadi mkubwa wa fasihi wa mwandishi. Maelezo kuhusu maisha ya kila siku yanachukuliwa kama ni maelezo halisi ya maisha ya wakazi wa Beijing yalivyokuwa katika karne ya 18. Riwaya ya "Ndoto katika Jumba Jekundu" inakubalika kwa wote kuwa ni kilele cha utunzi katika fasihi ya kikale ya China.