"Jiangger"
中国国际广播电台

      
"Jiangger" ni utenzi wa kabila la Wamongolia na ulitokea katika karne ya 15 hadi 17.

Mhusika mkuu katika utenzi huo Jiangger, alipokuwa na miaka miwili wavamizi wakatili wa Mangusi waliishambulia sehemu ya maskani yao, wazazi wake waliuawa, Jiangger akawa yatima. Ili kulipiza kisasi kwa ajili ya wazazi wake, alipokuwa na umri wa miaka mitatu alianza kupigana vita huku na huko na alipokuwa na umri wa miaka saba alipata ushindi mkubwa, alichaguliwa kuwa kiongozi wa kabila lao. Lakini wavamizi wa Mangusi walikuwa hawakubali kushindwa, walikuwa mara kwa mara wakifanya uvamizi dhidi ya kabila la Jiangger. Jiangger aliwaongoza majemadari 35 na askari hodari elfu 8 na kuwashinda wavamizi. Jiangger kwa hekima yake alijenga nchi iliyotamanika. Kwamba watu wanaoishi katika nchi hiyo hawazeeki, mimea inastawi mwaka mzima. Wananchi wanaishi kwa furaha tele na kicheko cha furaha kinasikika kila mahali.

Utenzi huo ulimwelezea shujaa aliyependwa sana na watu wa kabila lake kwa akili zake na ushupavu wake. Huu ni utenzi wenye taathira kubwa kwa fasihi ya kabila la Wamongolia, hivi sasa ni utamaduni unaohifadhiwa na serikali ya China.