"Manasi"
中国国际广播电台

      
Utenzi "Manasi" ulitokea kati ya karne ya 9 hadi 10 mkoani Xinjiang. Manasi ni shujaa katika masimulizi ya mapokeo mkoani Xinjiang, ni hadithi inayoeleza Manasi alivyoongoza watu kupambana na watawala wa kabila jingine waliowanyanyasa na kupigania uhuru wa kabila lake. Utenzi huo una beti laki 2.1 na maneno milioni 20. Katika utenzi huo watu zaidi ya 100 walieleziwa ambao wako wazee waliomwunga mkono na marafiki, pia wako watu wabaya, mfalme, wahaini na mashetani.

Utenzi "Manasi" umetafsiriwa kwa Kichina kutoka lugha ya kikabila na baadhi ya sehemu za utanzi huo zilitafsiriwa kwa lugha za Kiingereza, Kifaransa na Kijapan. Kutokana na umaarufu wa utenzi huo UNESCO iliwahi kuamua mwaka 1995 kuwa ni "Mwaka wa Manasi Duniani".