Huangdi Apambana na Chiyou

中国国际广播电台


  Miaka elfu kadhaa iliyopita, kwenye bonde la Mto wa Huanghe yalikuwepo makabila mawili, watemi wa makabila hayo waliitwa Huangdi na Yandi, watemi hao wawili ni ndugu. Wakati huo alikuwepo mtemi mmoja wa kabila lililoko kwenye bonde la Mto wa Changjiang, aliyeitwa Chi You.

Mara kwa mara Chi You alikuwa anawaongoza watu wake kushambulia makabila mengine.

Siku moja Chi You alishambulia sehemu ya Yandi, ingawa Yandi alipigana naye kwa nguvu zote, lakini hakufui dafu. Yandi alimkimbilia Huangdi kuomba msaada. Huangdi alishirikisha makabila mengine kupambana na Chi You.

Mwanzoni, kutokana na kuwa na silaha nzuri Chi You alipata ushindi kwa urahisi. Huangdi aliwaalika wanyama wakali kushiriki katika vita. Chi You alishindwa vibaya na kukimbia.

Huangdi alimfukuza, njiani giza liliingia na upepo mkali ulianza kuvuma, mvua ya radi ilikuwa kubwa. Huangdi alishindwa umfukuza. Hiyo ilitokana na kuwa Chi You aliialika miungu ya upepo na mvua kumsaidia. Wakati huo Huangdi aliialika miungu ya kiangazi, ghafla upepo ulitulia na mvua ilisimama.

Hatimaye Chi You alitumia uganga kuleta ukungu mnene ili Huangdi apotee njia, lakini Huangdi alitumia nyota ya kaskazini kuelekeza njia yake.

Baada ya mapambano marefu, Huangdi aliwaua ndugu 81 wa Chi You na kumkamata Chi You akiwa hai. Ili Chi You asilete matata, Huangdi alikata mwili kwa sehemu mbili, na kuzizika sehemu hizo katika mahali tofauti ili zisiunganike na kufufuka tena.

Baada ya Chi You kuuawa, Huangdi alichora picha yake kwenye bendera ya kijeshi ili kuwatia moyo askari wake.

Huangdi alikuwa na elimu nyingi, aliwahi kubuni zana nyingi kama mikokoteni, mashua na nguo yenye rangi tano. Mke wa Huangdi alikuwa pia ni mvumbuzi. Aliwafunza namna ya kufuga funza wa hariri na kutengeneza kitambaa cha hariri, na alivumbua kibanda kinachoweza kuchukuliwa yaani mwanvuli.

Watu wa China ya kale walimheshimu sana Huangdi, na watu wa China wanaona Huangdi na Yandi ni mababu wa Wachina, wanasema wao ni wazawa wa Yan na Huang. Wachina walijenga kaburi la Huangdi, na kila mwaka katika majir ya Spring Wachina kutoka sehemu mbalimbali duniani wanakwenda kufanya tambiko mbele ya kaburi hilo.