Hadithi kuhusu Kasri la Potala
中国国际广播电台


      Kasri la Potala ni jengo Dini ya Buddha liliko kwenye paa la dunia, Tibet.

Kasri la Potala lilijengwa na mfalme wa Tibet Sonzanganbu katika karne ya saba kwa ajili ya kumkaribisha binti wa mfalme wa Enzi ya Tang Wen Cheng kuwa mke wake. Kasri hilo lilijengwa kwenye mlima wa Tibet.

Katikati ya kasri hilo kuna ukumbi wa kufanyia ibada, ndani ya ukumbi huo kuna sanamu za Sonzangambu, binti wa mfalme wa mfalme wa Enzi ya Tang, Wen Cheng.

Kasri la Potala ni jengo lenye mchanganyiko wa mitindo ya Dini ya Buddha, madhehebu ya Tibet na kabila la Wahan, na ni alama ya ndoa kati ya kabila la Watibet na kabila la Wahan katika miaka 1300 iliyopita

 

Katika karne ya saba, Sonzanganbu alikuwa mfalme wa Enzi ya Turufan huko Tibet, alikuwa mfalme anayewapenda raia wake na kufanya enzi yake iimarike siku hadi siku. Ili kuweka uhusiano mzuri na Enzi ya Tang na kuingiza utamaduni wa kimaendeleo, Songzanganbu aliamua kumposa binti wa mfalme wa Enzi ya Tang, Wen Cheng. Kwa sababu wakati huo madola mengine pia yalituma wajumbe kuleta posa kwa binti yake, mfalme wa Enzi ya Tang, Tang Taizong aliwatolea maswali matatu, mtu ambaye angejibu vizuri maswali yote matatu, atakubali kumwoza binti yake kwa huyo.

Swali la kwanza: Katika busatani kuna magogo matatu ambayo mviringo wa pande mbili ni sawa, upande gani ni shina? Songzanganbu alijibu, magogo yote yawekwe ndani ya maji, upande uliozama zaidi ndio upande wa shina, kwa sababu upande wa shina ni mzito zaidi.

Swali la pili: Mfalme alitoa jade moja, na ndani ya jade kuna kitundu kilichopinda pinda kutoka upande moja hadi upande mwingine. Mfalme alimtaka apitishe uzi. Songzangambu alipaka asali kwenye upande mmoja, na kufunga uzi kwenye kiuno cha siafu na kumtia upande mwingine, siafu huyo alitambaa kutoka upande mmoja na kutoka kutoka upande mwingine na uzi.

Swali la tatu: Farasi mmoja ana mtoto wake anayenyonya maziwa, anawezaje kutofautisha mama farasi na mtoto wake kati ya kundi la wafasi wengi?
Songzanganbu alitafakari, kisha akasema, farasi wakubwa na wadogo wafungwe ndani ya mazizi mawili, na siku ya pili wafunguliwe, mtoto wa farasi aliyekimbilia farasi mkubwa na kunyonya maziwa yake, hao ndio mama na mtoto.

Baada ya Sonzanganbu kujibu maswali yote hayo sawasawa, mfalme aliongeza swali jingine, alitaka kumtambulisha binti yake Wen Cheng kati ya wasichana wengi. Kabla ya hapo, Songzanganbu alipata habari kwamba Wen Cheng alipenda kutumia manukato inayowavutia nyuki. Katika siku ya kutofautisha binti wa mfalme na wasichana wengine, alitia nyuki nguoni, aliachia nyuki mbele ya wasichana, nyuki walimrukia Wen Cheng. Mfalme Tang Taizong aliona kuwa kweli Songzanganbu ni mwerevu sana, alikubali kumwoza binti yake.

Songzanganbu alifurahi sana, alijenga kasri lenye vyumba 999 kwa ajili ya kumkaribisha binti wa mfalme Wen Cheng, kasri hilo ndio Kasri la Potala.