Hadithi kuhusu Kasri la Kifalme Mjini Shenyang
中国国际广播电台


  Kasri la Kifalme mjini Shengyang ni kasri la pili kwa ukubwa likilinganishwa na Kasri la Kifalme la Beijing. Tofauti yake na kasri la Beijing ni kuwa mtindo wake wa majengo ni wa kabila la Waman.

Kasri la Kifalme la Mji wa Shenyang liko katikati ya mji huo, lilijengwa katika Enzi ya Qing (1616-1911). Wafalme wawili wa mwanzo wa Enzi ya Qing waliishi katika kasri hilo, na baadaye kabila la Waman lilipindua Enzi ya Ming na kuhamia mji mkuu wa Enzi ya Qing, Beijing, na kujenga Kasri la Kifalme la Beijing.

  

Kasri hili lina eneo la mita za mraba elfu 60, lina majengo zaidi ya 70 na vyumba zaidi ya 300. Ukumbi mkuu wa kasri hilo ni mahali pa kufanyia sherehe kubwa na kufanya kazi za serikali, kuna vibanda vikubwa 11 ndani ya kasri hilo, ambavyo vinamaanisha mahema ya kabila la Waman wanaoishi kwa ufugaji.

Mbele ya kasri kuna milingoti 7, na juu ya kila mlingoti kuna bakuli la risasi. Kutokana na mila ya kabila la Waman, wanapofanya tambiko walikuwa wanaweka chakula kwenye bakuli hilo ili kuwalisha ndege.

Ingawa kasri hilo lilijengwa kwa mtindo wa kabila la Waman, lakini lilipojengwa utamaduni wa kabila la Wahan ulikuwa umeanza kupokelewa na kabila hilo, kwa hiyo, ukumbi mkuu wa kasri hilo ulijengwa kwa mtindo wa kabila la Wahan ulipokuwa katika Enzi ya Song (960-1279).

Kasri hilo lilianza kujengwa mwaka 1625 na kukamilika baada ya miaka 10, na baadaye wafalme wa Enzi ya Qing walifanya ukarabati na kuongeza majengo katika muda wa miaka 150. kasri hilo lilichanganya sanaa za makabila ya Wahan, Waman, Wamongolia, Wahui na Watibet, ni alama ya muunganisho wa makabila ya China.