Vita kwenye Sehemu ya Chang Ping
中国国际广播电台


       Katika Kipindi cha Madola ya Kivita, karne ya nne K.K. kulikuwa na madola saba yenye nguvu, lakini kati ya madola hayo, dola lililokuwa na nguvu kubwa zaidi ni Dola la Qin, vita kwenye sehemu ya Chang Ping ndio vita vya mwisho kabla ya Dola la Qin kuunganisha China nzima.

Madola ya Han, Wei, Yan na Zhao yalikuwa ni madola jirani na Dola la Qin. Katika madola hayo manne Dola la Zhao lilikuwa na nguvu kubwa zaidi na Dola la Wei lilikuwa dhaifu. Mwaka 268 Dola Qin lilianza kushambulia Dola la Wei ili kulazimisha dola hilo litawaliwe na Dola la Qin, kisha Dola la Qin lilishambulia Dola la Han, mfalme wa Dola la Han aliogopa sana, alimtuma mjumbe wake kwenda Dola la Qin na kumwambia mfalme wa Qin kwamba Dola la Han limekubali kugawa wilaya ya Shangdang kwa Dola la Qin. Lakini mkuu wa wila ya Shangdang hakukubali kuikabidhi sehemu yake kwa Dola la Qin, badala yake alitaka kutoa sehemu yake kwa Dola la Zhao.

Kutokana na uroho wa ardhi, mfalme wa Dola la Zhao alipokea ardhi hiyo ya Shangdang. Mfalme wa Dola la Qin aliposikia habari hiyo alikasirika. Mwaka 261 alimwagiza jemadari Wang Gan kushambulia sehemu ya Shangdang. Lakini askari wa Dola la Zhao katika sehemu ya Shangdang walikuwa hawana nguvu ya kupigana na askari wa Dola la Qin. Wakati huo mfalme wa Dola la Zhao alimwagiza jemadari mwingine Lian Po kushambulia sehemu ya Chang Ping ya Dola la Qin ili kurudisha sehemu ya Shangdang.

Jeshi lililoongozwa na Lian Po lilifika kwenye sehemu ya Chang Ping na kuanza kushambulia jeshi la Dola la Qin. Lakini jeshi la Dola la Zhao lilishindwa mara kadhaa. Kutoka na hali hiyo jemadari Lian Po alibadilisha mbunu yake, kwamba badala ya kufanya mashambulizi, alijenga ngome nyingi za kujikinga. Hivyo majeshi ya Dola la Zhao na Qin yalikabiliana.

Ili kuteka haraka sehemu ya Chang Ping, mfalme wa Dola la Qin alituma mjumbe wake kwenda Dola la Zhao kutia fitina kati ya mfalme na jemadari Lian Po kwa kutoa fedha nyingi, huku alivumisha uzushi kuwa Lian Po alitulia bila kufanya mashambulizi akilenga kusalim amri kwa jeshi la Qin. Siku chache mfalme wa Dola la Zhao alimrudisha Lian Po na kutuma jemadari mwingine Zhao Kuo huko Chang Ping.

Zhao Kuo ni jemadari asiyekuwa na uzoefu, uhodari wake ni kuongea tu mbinu za vita. Baada ya kufika kwenye sehemu ya Chang Ping alibadilisha mbinu ya Lian Po na kuandaa kufanya ushambulizi.

Mfalme wa Dola la Qin aliona kuwa hila yake ya kutia fitina ilifanikiwa, mara alimwagiza jemadari wake hodari Bai Qi badala ya Wang Gan huku aliamrisha askari wote wasitoboe siri hiyo.

Bai Qi alitumia hila ya kuondoa askari wake ili Zhao Kuo awafukuzie na baada ya askari wa Zhao Kuo kuingia kwenye sehemu waliyoacha kuwavamia kwa pande zote.

Mwaka 260, Zhao Kuo alianza kushambulia jeshi la Qin, askari waliotangulia wa Dola la Qin walijidai kushindwa na kurudi nyuma. Zhao Kuo hakufahamu kwamba hii ni hila, akaongoza askari wake kuwafukuza, walipofika kwenye sehemu iliyoficha askari wa Qin mara walivamiwa kwa pande zote. Zhao Kuo alitaka kurudi nyumba, lakini alishambuliwa na askari wa Qin waliokuwa wamejificha zamani.

Jemadari Zhao Kuo aliuawa kwa mshale, askari waliopoteza jemadari walikimbia ovyo. Jeshi la Dola la Qin lilipata ushindi mkubwa.

Vita vya Chang Ping vinajulikana sana katika historia ya vita nchini China.