Liu Bang
中国国际广播电台


Liu Bang ni mwanzilishi wa Enzi ya Han Magharibi (206 K.K.—220).

Liu Ban alizaliwa katika ukoo wa wakulima, mwanzoni aliwahi kuwa ofisa mdogo katika Enzi ya Qin, kwa sababu aliwaachia wafungwa huru alitorokea mbali na kujificha ili kukwepa adhabu ya mfalme wa Qin. Mwaka 209 aliwakusanya wakulima wa maskani yake kujiunga na jeshi la uasi lililoongozwa na Chen Sheng na Wu Guang. Baadaye jeshi aliloongoza lilitangulia kufika kwenye mji mkuu wa Enzi ya Qin, Xianyang, na kumaliza utawala wa Enzi ya Qin. Katika mji mkuu wa Qin alifuta sheria na kodi na kuweka kanuni “aliyeua mtu auliwe, aliyejeruhi mtu au kuiba aadhibiwe”. Kutokana na hayo alikaribishwa na raia.

Tokea hapo, Liu Bang alipambana na jeshi la Xiang Yu kwa miaka minne. Mwaka 202 jeshi la Liu Bang lenye askari laki tatu lilizunguka jeshi la Xiang Yu, Xiang Yu alijiua, Liu Bang alipata ushindi kamili na katika mwaka 202 alikuwa mwalme wa Enzi yake Han Magharibi.

Liu Bang alikuwa hodari wa kuchagua wasaidizi wake ambao mara nyingi walimsaidia kusalimika katika hatari. Hali iliyokuwa hatari kubwa ni kushiriki kwenye karamu ya Hong Men iliyoandaliwa na Xiang Yu. Wakati huo jeshi la Xiang Yu lilikuwa na nguvu kubwa kuliko jeshi la Liu Bang na Xiang Yu alitamani kumwangamiza Liu Bang na kuwa mfalme. Baada ya kufahamu hali hiyo Liu Bang alikwenda kwenye karamu akiwa pamoja na mshauri wake Zhang Liang. Kwenye karamu, jemadari wa Xiang Yu alijitokea kwa kucheza kitara kwa kisingizio cha kuchangia furaha ya karamu akitaka kumwua Liu Bang. Mshauri Zhang Liang aliona hali ilikuwa hatari, alimwamuru askari kumlinda. Dakika chache baadaye Liu Bang alitumia kisingizio cha kwenda chooni alitoroka na kurudi kwa siri. Kisha mshauri wake aliingia kwenye ukumbi wa karamu na kutoa zawadi kwa Xiang Yu, na kumwambia Xiang Yu kuwa Liu Bang keshaondoka. Baadaye Liu Bang alikusanya nguvu zake zote kulishinda kabisa jeshi la Xiang Yu na kuansisha Enzi ya Han Magharibi.

Baada ya kuwa mfalme, Liu Bang alitunga sera nyingi za kuendeleza uzalishaji. Kutokana na vita vya miaka mingi, idadi ya watu ilipungua, aliwaachia wafungwa na watumwa huru, aliwaachia askari wake warudi nyumbani kushughulika na kilimo.

Liu Bang alibeza wasomi, aliona kuwa utawala wake ulipatikana kwa vita, mashairi na vitabu kwake vilikuwa havina maana. Waziri wake Lu Jia alisema, “Kitu kilichopatikana kutoka mgongo wa farasi kinaweza kutumika katika utawala?” Kusikia hayo alimwagiza Lu Jia aandike kitabu cha kueleza sababu za enzi iliyotangulia kushindwa ili kuboresha utawala wake. Liu Bang alikaa madarakani kwa miaka 12, katika mapambano dhidi ya waasi alipigwa mshale, baada ya kuugua muda alikufa.