Da Yu
中国国际广播电台


Miaka 4000 iliyopita mafuriko makubwa yalitokea katika sehemu za bonde la Mto Huanghe. Kutokana na mchango wa kuondoa mafuriko, Da Yu aliheshimiwa sana miongoni mwa raia, mtemi wa kabila la Wachina Shun alimwachia nafasi yake. Hadithi kuhusu Da Yu ilielezwa kizadi hadi kizazi.

Inasemekana kwamba katika miaka Yao alipokuwa madarakani mafuriko yaliyokea, maji yaligharisha mimea na nyumba, watemi wa makabila yote walimchagua baba wa Da Yu kwenda kupambana na mafuriko. Baada ya miaka tisa kupita mafuriko yaliendelea, baba yake aliuawa kwa adhabu na mtoto wake Da Yu aliagizwa kupambana na mafuriko.

Da Yu hakufuata baba yake alivyopambana na mafuriko, bali alichimba mifereji na kuyaongoza maji baharini. Da Yu alifanya kazi sawa na raia, kwa juhudi za miaka 13 mwishowe alifanikiwa kuyapeleka mafuriko kwenye bahari.

Da Yu alianza kupambana na mafuriko baada ya siku chache kuoa. Siku moja alipopita mbele ya nyumbani alisikia kilio cha mtoto wake mchanga, lakini hakuingia nyumbani kutokana na shughuli.

Kutokana na mchango wake mkubwa wa kuondoa mafuriko, watu walimchagua kuwa kiongozi wa muungano wa makabila.

Baadaye kabila la Da Yu lilimpendekeza mtoto wa Da Yu, aliyeitwa Qi, kurithi kiti cha Da Yu, tokea hapo utaratibu wa uchaguzi wa muungano wa makabila ulifutwa na badala yake utaratibu wa kurithisha kiti cha ufalme ulitokea.

Enzi ya kwanza ya kifalme, Xia, ilitokea katika mfumo wa jamii ya utumwa nchini China.