中国国际广播电台
Kiasi
cha miaka 4000 iliyopita,
walitokea watu kadhaa mashuhuri,
Yao, Shun, Da Yu na wengine.
Yao na Shun walikuwa ni wafalme
wawili wa mwanzo kabisa nchini
China katika masimulizi ya
mapokeo, watu hao wawili ndio
walioanzisha historia ya China.
Katika vitabu vingi vya hekaya
na masimulizi ya mapokeo,
kuna mengi yaliyoeleza kuhusu
Yao na Shun.
Yao alikuwa ni mtemi mwishoni
mwa jamii ya kiasili, ni mwakilishi
wa utamaduni wa mwanzo kabisa
nchini China. Kutokana na
masimjulizi ya mapokeo, Yao
alikuwa ni kizazi cha babu
wa taifa la China Huangdi,
alikuwa mtu mwenye akili,
roho nzuri na aliheshimiwa
sana. Alipokuwa na umri wa
miaka 16 aliendekezwa kuwa
mtemi. Watu wa kabila la Yao
waliishi katika sehemu ya
kaskazini ya China, mji wa
Baoding mkoani Hebei wa sasa.
Kwa kushirikisha makabila
mengine yaliyoko katika sehemu
yake alipigana na wavamizi
na kuwapokea kuwa watu wa
kabila lake. Kutokana na nguvu
za kabila lake kuongezeka
haraka, Yao alikuwa mkuu wa
muungano wa makabila kadhaa,
watu wa baadaye walimwita
mfalme Yao.
Yao alikuwa mfalme mwema,
aliishi kama raia wa kawaida
na kutenda mambo kwa uadilifu.
Alithamini sana maofisa walio
wema, alikagua maofisa wake
kazi walizofanya na kuwasifu
wale walio bora na kuwaadibu
walio wabaya. Kutokana na
hayo, kazi za utawala wake
zilikuwa na utaratibu mwema.
Aliweka ofisa wa unajimu ili
watu waweze kushughulika na
kilimo kwa misimu, watu wa
kale wa China walisema, kipindi
cha utawala wa Yao kilikuwa
kipindi cha maendeleo ya haraka
katika kilimo. Yao alikuwa
anatilia maanani sana uhusiano
mwema kati ya makabila na
kuwashawishi watu wake waishi
kwa majirani wema, hali ya
jamii ilikuwa tulivu na ilijaa
upendo.
Yao alikuwa madarakani kwa
miaka 70, alikuwa mfalme wa
kwanza kabisa kumwachia mrithi
wake kiti cha ufalme kwa mujibu
wa uhodari wa mtu.
Inasemekana kwamba aliwataka
watu na maafisa wa sehemu
mbalimbali wawapendekeze watu
walio hodari, hata mtu huyo
akiwa hana hadhi katika jamii.
Mwishowe watu walimpendekeza
mtu mmoja maskini aliyeitwa
Shun. Inasemekana kwamba wazazi
walikuwa wakali kwa Shun na
ndugu zake pia walikukwa wajeuri
kwa Shun, lakini Shun aliishi
nao vema. Watu waliona kuwa
Shun ni mtoto mwema kwa wazizi
na ni mwenye maadili mema,
alistahili kuwa mtawala na
anaweza kuongoza vivuri taifa.
Yao alimchunguza kwa pande
zote, aliona kuwa Shun kweli
ni mtu mwenye maadili mema
na pia ni hodari. Baada ya
miaka mitatu alimwachia Shun
kiti chake cha ufalme badala
ya kumwachia mtoto wake Dan
Zhu. Kitendo hicho kisichokuwa
na tamaa binafsi kwa ajili
ya maslahi ya wananchi, kinasifiwa
kuwa ni demokrasia ya mwanzoni
kabisa nchini China.
Baada ya kuwa mfalme, Shun
alistawisha zaidi siasa ya
demokrasia. Alitunga sheria
ya adabu na adhabu, aliwateua
maofisa wa kazi mbalimbali
kusimamia mambo ya utawala,
uchumi, elimu, shughuli za
bidhaa za kazi ya mikono,
muziki, na pia alitunga sheria
ya kuwachunguza maofisa, hivyo
utaratibu wa utawala wa taifa
ulizidi kukamilika kwa kiasi
kikubwa.
Shu alitilia mkazo katika
uzalishaji, uchimbaji wa mifereji
na visima, na kuweka urafiki
na watu wengi. Katika kipindi
cha utawala wa Shun kilimo
na ufundi vyote vilipata maendeleo
ya kasi. Shun alikuwa mfano
wa maadili mema kwa vitendo,
alishirikiana na wananchi
katika dhiki na faraja. Katika
kipindi cha utawala wake watu
walikuwa na maadili mema,
watiifu, na waliishi bila
usumbufu, kipindi chake kilikuwa
kipindi chenye siasa bora,
uzalishaji mkubwa na ustawi
wa muziki. Kuhusu urithi wa
kiti cha ufalme, Shun pia
alitumia njia kama ya mfalme
Yao, alimwachia kiti chake
Yu (Da Yu), mtu aliyetoka
mchango mkubwa katika shughuli
za kupambana na mafuriko.
|