Shen Nong (Yandi)
中国国际广播电台


Miaka 5000 iliyopita, Shen Nong alikuwa mtemi wa kabila moja. Katika zama za kale, mtemi alikuwa sawa na watu wa kawaida kufanya kazi mashambani, na alipokuwa analima alivumbua plau ambayo ilisaidia sana kwenye maendeleo ya kilimo. Kutokana na mchango wake huo watu walimwita Shen Nong (mkulima hodari).

Zama alipoishi Shen Nong zilikuwa ni kipindi cha mwanzo wa komuna ya ubaba, kulikuwa hakuna unyonyaji wala ukandamizaji, watu wote walikuwa sawa. Kutoka na maandishi ya kale, katika zama hizo wanaume walifanya kazi shambani na wanawake walifuma vitambaa, kulikuwa hakuna gereza wala adhabu, wala kulikuwa hakuna jeshi wala polisi.

Shen Nong pia alikuwa mtaalamu wa dawa wa mwanzo kabisa nchini China. Inasemekana kwamba aliona usumbufu sana alipoona watu wanavyougua. Alifikiri kwamba mazao yanaweza kusaidia afya basi majani na mizizi pengine inaweza kusaidia kuondoa ugonjwa. Katika masimulizi ya mapokeo, Shen Nong alichuma aina mbalimbali za mimea na kuonja, na alikuwa mara kwa mara alipatwa na sumu. Aliwahi kuandika kitabu cha “Dawa za Mitishamba za Shen Nong”, kikieleza maelezo ya tiba ya magonjwa.

Kadhalika, Shen Nong pia alikuwa mnajimu kwa ajili ya kukumbuka mambo na kupiga ramli. Zaidi ya hayo, alipoona watu wanaolima mazao mengi kuliko mahitaji, na baadhi ya mazao wanayohitaji walikuwa hawajui kulima, aliweka mahali maalumu kwa ajili ya kubadilishana mazao, hivyo kulitokea soko.

Shen Nong alikuwa madarakani miaka 140, baadaye Huandi alichukua nafasi yake. Alizikwa katika mji wa Changsha wa leo, mpaka sasa kuna kaburi lake, watu wanaliita kaburi lake kuwa kaburi la Yandi.