中国国际广播电台
Hanfeizi
aliishi katika Enzi ya Vita
vya Kivita (475 K.K.—221K.K.),
alikuwa ni mwanafalsafa, na
mwanasheria. Alikuwa wa kwanza
kutoa nadharia ya kisheria
kwa ajili ya utawala taifa
wenye kiini kimoja.
Hanfeizi aliishi katika
karne ya tatu ambapo ilikuwa
ni kipindi cha mwisho cha
Enzi ya Kivita. Alikuwa na
kigugumizi, hakuwa hodari
wa kusema, lakinialikuwa ni
hodari wa kuandika vitabu.
Kitabu alichoandika “Hanfeizi”
kilikusanya maandishi yote
ya wanasheria wa Enzi ya Qin.
Kitabu hicho kinachopatikana
sasa kina makala 55 zenye
maneno zaidi ya laki moja,
na makala nyingi ni zake mwenyewe.
Alitetea siasa ya kutoa zawadi
kubwa kwa watu waliokuwa na
mchango na kutoa adhabu kali
kwa watu waliokuwa wahalifu,
na kutilia maanani kilimo
na nguvu za kupigana vita.
Kadhalika alitetea kuwa madaraka
ya mfalme yanawakilisha nia
ya mungu. Tokea Enzi ya Qin
yenye utawala wa kidikteta
katika jamii ya kiumwinyi
nadharia ya Hanfeizi ilikuwa
na athari kubwa.
|