Zhuangzi
中国国际广播电台


Zhuangzi aliishi katika karne ya nne katika dola la Song, aliwahi kuwa ofisa mdogo, alikuwa mwenye akili na aliwahi kutembelea kila mahali. Kutokana na werevu wake aliwahi kualikwa na mfalme wa Dola la Chu, lakini alikataa na tokea hapo hakuwahi kuwa ofisa, alijitenga na jamii na kuishi kwa kusuka viatu kwa majani. Inasemekana kwamba aliandika vitabu vyenye maneno zaidi ya laki moja.

Zhuangzi aliona kuwa maisha ya binadamu lazima yawe ya uhuru kabisa wala sio kuwa na mali nyingi au sifa za bure.

Pamoja na fikra za Zhouyi, Laozi, fikra za Zhuangzi pia zilikuwa athari kubwa katika Enzi ya Tang (618—907).

Fikra za Zhuangzi hazielezwi kwa nadharia tupu bali kwa hekaya. Kitabu chake kilikuwa kama ni mkusanyiko wa hekaya.