Mencius
中国国际广播电台


Mencius alikuwa ni mwanafikra mkubwa, aliishi Enzi ya Madola ya Kivita (karne ya 5 K.K. hadi karne ya 3 K.K.) ni mmoja wa wawakilishi wa fikra za Confucius nchini China.

Mencius alirithi na kuendeleza fikra za Confucius, alikuwa ametofautisha wazi tabaka la watawala na tabaka la watawaliwa, alisema kuwa “wanaofanya kazi kwa akili wanatawala, na waliofanya kazi kwa nguvu za mwili wanatawaliwa” na aliweka matabaka toka mfalme hadi makabwera. Na wakati huo alitetea kuwa uhusiano kati ya watawala na watawaliwa kama ni wazazi na watoto, na kusema kwamba watawala wawatendee vema raia kama wazazi wao na raia wawatii watawala kama wanavyowatii wazazi wao.

Mencius aliunganisha nadharia yake pamoja na siasa. Alisisitiza kuwa maadili mema ni msingi wa siasa. Alisema, “utawala ni msingi wa taifa, na msingi wa taifa ni familia, na msingi wa familia ni maadili ya kila mmoja.” Alisema kuwa kama kila mmoja aliwatendea wengine kwa maadili mema, utawala wa kimnwinyi unahakikishwa.

Ili kufahamisha nadharia yake alisema, asili ya binadamu ni utu, aliona kuwa ingawa kuna tofauti ya kazi na watu wanaishi katika matabaka tofauti, lakini utu ni mmoja.

Ingawa fikra za Mencius zilikuwa na athari kubwa katika historia ya China katika siasa, fikra, utamaduni na maadili, lakini haikuthaminiwa na mtawala wa enzi yake.