中国国际广播电台
Laozi,
jina lake la ukoo ni Li na
jina lake ni Er, jina Laozi
ni jina lake alilopewa na
watu kwa heshima. Alikuwa
mtu wa Dola la Chu katika
Enzi ya Spring na Autumn (770
K.K.—476 K.K.). inasemekana
kwamba yeye alikuwa ni mtu
mrefu mwenye masikio makubwa,
kipaji kipana na midomo minene.
Aliwahi kuwa mtunza vitabu,
na kutokana na kazi hiyo alikuwa
na elimu kubwa. Confucius
aliwahi kwenda kukutana naye
kutaka kujifunza. Laozi aliandika
kitabu cha “Maadili”, kitabu
hicho kilikuwa na maneno elfu
tano. Katika kitabu hicho
aliandika kwamba mambo yote
duniani yanahusiana na kusaidiana.
Na pia katika kitabu hicho
alieleza kuwa mambo yanaweza
kubadilika, kwamba mambo mazuri
yanaweza kubadilika kuwa mambo
mabaya na mambo mabaya yanaweza
kubadilika kuwa mazuri, na
ndani ya mambo mazuri kuna
sehemu ya kuyafanya mambo
mazuri kuwa mabaya na ndani
ya mambo mabaya kuna sehemu
fulani ya kuyafanya mambo
mabaya kuwa mambo mazuri.
Alisema mbegu ndogo inaweza
kuchipuka na kua kuwa mti
mkubwa, chembe za udongo zinaweza
kujenga jukwaa kubwa. Alisema
watu haifai kutishika na taabu,
ili mradi tu akiwa na nia
ya kufanya juhudi kutoka kazi
ndogo ndogo bila kuacha atapata
mafanikio makubwa.
Laozi alipinga sana vita.
Alisema, mahali palipokuwa
na vita patakuwa vichaka,
na baada ya vita hakika kutakuwa
na maafa ya kilimo, na pia
alipinga watawala kuishi maisha
ya anasa na kutoza kodi kupita
kiasi.
Fikra za Laozi ni muhimu
katika historia ya falsafa
ya China, na fikra zake zilikuwa
na taathira kubwa kwa wanafikra
wa kimaendeleo na wanamageuzi
ya jamii.
|