中国国际广播电台
Tiba
ya jadi ya Kichina ina historia
ndefu, na walitokea wataalamu
wengi wa dawa. Katika karne
ya 16, Enzi ya Ming nchini
China, alikuweko mtu mmoja
mashuhuri wa dawa za mitishamba
aliyeitwa Li Shizhen. Kitabu
maarufu cha “Tiba na Dawa
za Mitishamba” ndicho kilichoandikwa
naye.
Li Shizhen (1518—1593) alizaliwa
katika mkoa wa Hubei. Baba
wa Li Shizhen alikuwa mganga,
na Li Shizhen alipokuwa mtoto
mara kwa mara alifuatana na
baba yake kwenda milimani
kutafuta dawa za mitishamba
na kutengeneza dawa nyumbani.
Lakini kutokana na kuwa hadhi
ya waganga ilikuwa duni katika
jamii, Li Shizhen aliamua
kusoma ili apate nafasi ya
ofisa.
Mwaka 1531, Li Shizhen alipokuwa
na umri wa miaka 14 alifanikiwa
katika mtihani wa wilaya,
baadaye aliwahi kushiriki
mitihani ya taifa kwa mara
tatu lakini mara zote alishindwa.
Tokea hapo alianza kujifunza
udaktari kutoka kwa baba yake.
Ili kujipatia elimu nyingi
alikuwa mara kwa mara anazungumza
na wavuvi, wawindaji, watema
kuni na wakulima ili kukusanya
tiba za kienyeji, na kwa kufanya
majaribio alielewa kazi ya
tiba ya kila aina ya mitishamba.
Mwaka 1522, Li Shizhen alipokuwa
na umri wa miaka 35 aliandika
kitabu chake “Tiba na Dawa
za Mitishamba”.
Kitabu cha “Tiba na Dawa
za Mitishamba” kimekusanya
dawa za mitishamba aina 1892
na aina za matibabu zaidi
ya elfu 11, na pia kuna picha
za mimea ili watu watambue
vilivyo mimea yenyewe.
Li Shizhen alitumia maisha
yake yote katika ukusanyaji
uzoefu wa matumizi ya dawa
za mitishamba miongoni mwa
watu wa China na aliandika
kitabu cha “Tiba na Dawa za
Mitishamba”. Kitabu hicho
kilichapwa mara kadhaa nchini
Japan na pia kilitafsiriwa
kwa lugha za Kiingereza, Kifaransa,
Kijerumani na Kilatini, kilienea
duniani kote tokea karne ya
17.
|