Mnajimu Zhang Heng
中国国际广播电台


Zhang Heng alizaliwa mkoani Henan, alipokuwa mtoto alipenda sana kujifunza na kuandika insha na alipokuwa na miaka 17 alifika mji wa Changan ambao uliwahi kuwa mji mkuu wa enzi nyingi katika historia ya China, alipokuwa huko alifanya uchunguzi wa kumbukumbu za kale, mila na desturi za wenyeji na hali ya uchumi ya jamii, kisha baadaye alichaguliwa kuwa ofisa katika mji wa Luoyang, ambao ulikuwa mji mkuu katika miaka yake. Lakini kutokana na hamu yake na unajimu kwa mara mbili aliacha kazi yake ya ofisa na alitumia miaka mitatu kufanya utafiti kuhusu falsafa, hisabati, unajimu na alipata elimu nyingi.

Katika miaka elfu mbili iliyopita, elimu kuhusu ulimwengu zilikuwa nyingi. Zhang He aliona kuwa ulimwengu ni kama yai, dunia ni kama kiini cha yai, mbingu ni kubwa na dunia ni ndogo, na aliona kuwa kabla kutengana kwa mbingu na ardhi, dunia ilikuwa ya mchanganyiko wa vitu vyote, na baada ya kutengana, vitu vyepesi vilipaa juu na vitu vizito vilibaki chini na kuwa dunia. Aliweza kueleza mwendo tofauti wa sayari kutokana na umbali tofauti na jua, sayansi ya zama hizi imethibitisha kuwa mwendo wa sayari unahusika na umbali na jua, kwa hiyo mtazamo wa Zhang He ulikuwa sawa.

Zhang He alibuni kifaa cha kupima tetemeko la ardhi, kifaa hicho ni cha mwanzo kabisa duniani. Mwaka 138 kifaa hicho kilitoa habari ya tetemeko la ardhi lililotokea katika mkoa wa Shanxi.

Zhang Heng licha ya kuwa mnajimu, naye pia alikuwa mwanafasihi na mchoraji. Kutokana na maandishi ya kale, Zhang Heng alituachia maandishi yake 32 kuhusu sayansi, falsafa na fasihi. Na kati ya makala hayo yako makala ya kueleza msimamo wake wa siasa, kuna makala inayoeleza matumaini ya binadamu kusafiri katika sayari nyingine na kuna makala inayoeleza mandhari ya miji.