中国国际广播电台
Watu
wanapougua wanakwenda kuonana
na daktari wakitumai kupona,
lakini kama ugonjwa ukiwa
sugu,watu hao husema “laiti
daktari ajabu Huatuo angekuwa
hai”. Huyu Huatuo alikuwa
mganga wa miaka zaidi ya elfu
mbili iliyopita, kutokana
na uhodari wake watu walimmsifu
kuwa ni “daktari wa ajabu”.
Huatuo alikuwa ni mwenyeji
wa mkoa wa Anhui, tarehe yake
ya kuzaliwa haiwezi kuthibitishwa,
lakini aliuawa kabla ya mwaka
208. Inasemekana kwamba Huatuo
alikuwa na afya nzuri na alipokuwa
na umri wa miaka mia moja
afya yake bado ilikuwa njema.
Kutokana na maandishi ya historia,
alikuwa mganga wa kienyeji
na alikuwa na nafasi nyingi
za kuwa ofisa, lakini alikataa.
Jemadari mkubwa Cao Cao (155-220)
alikuwa na ugonjwa wa kuumwa
na kichwa kwa muda mrefu,
alimwomba Huatuo amtibu, muda
si mrefu Cao Cao alipona kabisa.
Tokea hapo Cao Cao alimlazimisha
Huatuo aishi naye na kutunza
afya yake. Lakini siku chache
baadaye Huatuo alirudi nyumbani
kwa kisingizio kuwa mkewe
alikuwa anaumwa. Ingawa Cao
Cao alimhimiza mara kadhaa
arudi kwake, lakini Huatuo
hakurudi. Cao Cao aliamua
kumtia gerezani na baada ya
muda alimwua.
Huatuo alikuwa na elimu nyingi
za tiba ambazo zinahusika
na magonjwa ya maambukizi,
minyoo, wanawake na watoto,
mfumo wa kupumua na ngozi,
na hasa elimu ya kufa ganzi
kwa mwili mzima na upasuaji.
Huatuo alikuwa mtu anayependwa
sana na watu, kwa kiasi fulani
uhodari wake katika matibabu
umeonesha maendeleo ya tiba
katika miaka elfu mbili iliyopita
nchini China. Huatuo alikuwa
mmoja wa watu waliotangulia
kutumia dawa za ganzi duniani.
Huatuo alikuwa hodari wa
kufanya upasuaji. Aliwahi
kumfanyia upasuaji msichana
mmoja mwenye umri wa miaka
20 ambaye alikuwa na kidonda
kwenye goti kwa miaka minane.
Huatuo alifunika dawa ya unga
kwenye kidonda baada ya kutoa
kipande kimoja cha mfupa,
msichana huyo alipona baada
ya siku saba. Watu wa leo
wanaona kuwa kipande cha mfupa
alichotoa kilikuwa ni kipande
kilichokufa. Kulikuwa na mgonjwa
mwingine mzee ambaye alikwenda
kumwona, baada ya kuchunguza
ugonjwa wake Huatuo alimwambia
kuwa ugonjwa wake umekuwa
mkubwa na anaweza tu kufayiwa
upasuaji wa tumbo, lakini
hata hivyo, anaweza kuishi
kwa miaka 10 hivi, na bila
ya upasuaji pia ataishi muda
huo huo, kwa hiyo ni afadhali
aache upasuaji. Lakini kutokana
na usumbufu wa ugonjwa wenyewe
alimwomba Huatuo amfanyie
upasuaji, maumivu yalipungua
lakini mzee huyo hakuishi
zaidi ya miaka 10.
Huatuo pia alikuwa hodari
wa kugundua ugonjwa kwa kuangalia
sura ya mtu. Siku moja alipokuwa
katika baa, aliwaona watu
kadhaa wakinywa pombe, aligundua
mmoja kati yao alikuwa na
ugonjwa mkubwa, alimwambia
asinywe zaidi na kurudi nyumbani
haraka. Mtu huyo alipokuwa
njiani alianguka kutoka kwenye
gari na baada ya kufika nyumbani
siku chache alikufa.
Watu wa leo wanatilia maanani
sana mazoezi ya kuimarisha
afya. Miaka elfu mbili iliyopita
Huatuo alivuni mazoezi mepesi
ili kuimarisha afya, “mchezo
wa wanyama wa aina tano” ambayo
yalikuwa ni mazoezi mepesi
kwa vitendo vya aina tano
za wanyama: chui, swala, dubu,
nyani na ndege. Watu wanaofanya
mchezo huo wananyoosha mishipa,
kuongeza mzunguko wa damu,
kuongeza uwezo wa kujikinga
na maradhi. Wanafunzi wa Huatuo
walikuwa wengi, na kati yao
watatu walikuwa maarufu ambao
walitoa mchango mkubwa katika
tiba ya Kichina. Baada ya
Huatuo kufariki, watu walimjengea
mahekalu mengi kumkumbuka
katika mahali alipowahi kutoa
matibabu.
|