Chen Sheng na Wu Guang Wafanya Uasi
中国国际广播电台


      
Chen Sheng na Wu Guang walikuwa ni viongozi mashuhuri wa uasi wa wakulima, uasi ulioongozwa nao ulikuwa mkubwa na wa kwanza katika historia ya China ambao ulizuka katika karne ya tatu mwishoni mwa Enzi ya Qin.

Mwaka 210 mfalme wa kwanza wa Enzi ya Qin alifariki, mtoto wake Hu Hai alirithi kiti cha ufalme.

Mfalme Hu Hai alikuwa mpumbavu, chini ya utawala wake raia waliishi vibaya na kutozwa kodi nyingi.

Mwaka 209 mfalme Hu Hai aliamuru wakulima 900 kwenda kulinda mji wa Yu Yang (wilaya ya Miyun karibu na Beijing).

Chen Sheng aliteuliwa kuwa kiongozi wa wakulima hao. Lakini walipokuwa njiani walizuiliwa na mvua kubwa, walikuwa hawawezi kufika mji wa Yu Yang kwa wakati uliopangwa. Kutokana sheria, wangechelewa wote wangeuawa. Chen Sheng na Wu Guang aliwaambia wakulima kuwa ni afadhali kufanya uasi kuliko kuuawa. Wakulima hao waliwachagua Cheng Sheng kuwa jemadari na Wu Guang kuwa msaidizi wake na kuunda jeshi la kwanza la wakulima katika historia ya China.

Katika muda mfupi jeshi hilo liliteka miji sita mikuu ya wilaya na popote jeshi hilo lilipopita raia waliliunga mkono na kujiunga nalo. Jeshi hilo lilikuwa na askari wengi siku hadi siku na kuwa jeshi kubwa lenye askari laki kadhaa.

Jeshi hilo liligawanyika katika sehemu tatu, wakati jeshi hilo lilipokuwa na askari laki kadhaa walianza kushambulia mji mkuu wa Enzi ya Qin.

Mfalme Hu Hai alishikwa na hofu wakati jeshi la Cheng Sheng na Wu Guang lilipokaribia mji mkuu, alihamisha askari laki kadhaa kuja mji mkuu na kushirikiana na jeshi la kifalme kupambana na jeshi la uasi kutoka mbele na nyuma, na Wu Guang aliuawa. Mwezi Desemba mwaka 209 Cheng Sheng pia aliuawa katika pambano kali na jeshi la Enzi ya Qin.

Ingawa viongozi wa uasi huo Chen Sheng na Wu Guang wate waliuawa, lakini askari wao walijiunga na jeshi jingine lililoongozwa na Xiang Yu na Liu Bang na kuendelea kupambana na jeshi la Enzi ya Qin. Mwaka 206 Enzi ya Qin iliangushwa na jeshi la uasi la wakulima.